Pafnusi wa Tebe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Pafnusi wa Misri (karne ya 16 au 17).

Pafnusi wa Tebe alikuwa mmonaki mfuasi wa Antoni Mkuu na wa Makari Mkuu, halafu askofu wa mji fulani wa Thebaid kaskazini (Misri) mwanzoni mwa karne ya 4.

Wataalamu wengine wanamhesabu kati ya wahusika muhimu wa Mtaguso wa kwanza wa Nisea (325), na wanasema aliongozana na Atanasi wa Aleksandria kushiriki Sinodi ya kwanza ya Turo (335).

Kabla ya hapo alidhulumiwa na serikali ya Dola la Roma akakatwa mguu wa kushoto na kuharibiwa jicho la kulia kwa sababu ya imani yake. Pia alipelekwa kufanya kazi migodini.

Tangu zamani anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 19 Aprili [1]; katika Kanisa la Kilatini tarehe 11 Septemba[2][3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo kwa Kiswahili[hariri | hariri chanzo]

  • Misemo ya Mababa wa Jangwani (Apophthegmata Patrum) – tafsiri ya W. Ngowi, O.F.M.Cap. – ed. Salvatorianum – Morogoro 2000ISBN 0-264-66350-0

Marejeo mengine[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.