Nikanori mwinjilisti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mchoro wa ukutani wa Fra Angelico, ukionyesha Mtume Petro akiweka wakfu wainjilisti saba wa kwanza.

Nikanori mwinjilisti (alifariki Kupro, 76) ni Myahudi wa karne ya 1 anayejulikana hasa kutokana na Matendo ya Mitume.

Anaheshimiwa na madhehebu mbalimbali ya Ukristo kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa na Kanisa Katoliki na Anglikana tarehe 28 Julai pamoja na wenzake Prokoro, Timone, Parmena na Nikola wa Antiokia[1][2].

Katika Biblia[hariri | hariri chanzo]

Alikuwa mmojawapo kati ya wanaume saba wa lugha ya Kigiriki katika Kanisa mama la Yerusalemu ambao, wakiwa wamejaa Roho Mtakatifu na hekima, walichaguliwa na waumini wenzao wakawekewa mikono na Mitume wa Yesu ili kushughulikia kwa niaba yao huduma za fukara (Mdo 6)[3].

Katika mapokeo[hariri | hariri chanzo]

Mapokeo ya baadaye yanasimulia kwamba alikwenda Kupro na huko alifia dini yake.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. "Martyrologium Romanum", Typis Vaticanis, Editio Altera, 2004
  2. Calendar of saints (Episcopal Church in the United States of America)
  3. https://www.santiebeati.it/dettaglio/91953

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.