Etna

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mlima Etna)
Etna ikiwa na Catania chini yake.
Etna nyuma ya milima Peloritani.
Hoteli Sapienza, inayofikiwa na watalii wengi.
Theluji inatumika kwa mchezo wa skii.

Etna (kutoka Kilatini: Aetna; kwa Kiitalia pia Mongibello; kwa Kisisili Mungibeddu au â Muntagna) ni volkeno hai wa Sicilia mashariki (Italia visiwani) kati ya miji ya Catania na Messina. Ndiyo ndefu kuliko zote za Ulaya[1]: kwa sasa imefikia mita 3357 juu ya usawa wa bahari.[2]

Etna inaenea katika kilometa mraba 1190 ukiwa na duara ya km 140 miguuni pake. [3]

Etna inakadiriwa kuwa na miaka 350,000 - 500,000 na ni kati ya volkeno hai zaidi duniani, kwa kuwa haitulii karibu kamwe, lakini kwa namna yake si hatari. Lava yake inageuka baada ya miaka kadhaa kuwa nzuri sana kwa kilimo.

Mnamo Juni 2013 iliingizwa na UNESCO katika orodha ya urithi wa dunia.[4]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Italia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Etna kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.