Mikrobiolojia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Agar plate iliyojaa vidubini.

Mikrobiolojia (kutoka maneno ya Kigirikiμῑκρος, mīkros, "ndogo"; βίος, bios, "uhai"; na λογία, logia, "elimu") ni fani inayochunguza vidubini vyenye seli moja, nyingi au visivyo nayo kabisa.[1] Mikrobiolojia ina matawi yake, yakiwemo virolojia, mukolojia, parasitolojia na bakteriolojia.

Antonie van Leeuwenhoek, mwanamikrobiolojia wa kwanza na mtu wa kwanza aliyeona bakteria kwa darubini.

Bakteria ziligunduliwa mara ya kwanza na Antonie van Leeuwenhoek mwaka wa 1676, kwa kutumia darubini ya lensi moja ya muundo wake mwenyewe.[2] Aliziita "animalcules" na alichapisha habari za utafiti wake kwenye msururu wa barua kwa Shirika la Muungano wa Mfalme.[3][4][5] Jina bacteriam lililetwa miaka mingi baadaye, na Christian Gottfried Ehrenberg katika mwaka wa 1838.[6]

Mwaka 1859 Louis Pasteur alionyesha kuwa mchakato wa kuchachusha unasababishwa na ukuaji wa vijiumbe, na kwamba ukuaji huu si wa kizazi cha kujianzia. (Hamira na kuvu, ambazo kwa kawaida zinahusishwa na uchachushaji, si bakteria, ila ukungu.) Pamoja na mwenzake, Robert Koch, Pasteur alikuwa wa kwanza kuitetea nadharia ya kijidudu ya ugonjwa.[7]

Robert Koch alikuwa mwanzilishi wa taaluma ya uuguzi wa mikrobiolojia na alishughulikia kipindupindu, kimeta na kifua kikuu. Katika utafiti wake wa kifua kikuu, Koch hatimaye alithibitisha nadharia ya kijidudu, ambayo ilimfanya atunukiwe Tuzo la Nobel mwaka wa 1905.[8] Katika madai yake, Koch aliweka vigezo vya kutathmini kama kiumbe ndicho husababisha ugonjwa, na madai haya yanatumika mpaka leo hii.[9]

Ingawa katika karne ya 19 ilijulikana kwamba bakteria ndizo chanzo cha magonjwa mengi, hakuna matibabu yoyote ya viua-bakteria yaliyopatikana.[10] Katika mwaka wa 1910, Paul Ehrlich alitengeneza kiua vijasumu cha kwanza, kwa kubadilisha rangi ambazo kwa kuchagua zilitia mawaa Treponema pallidum, spirokaeti ambayo husababisha kaswende katika mchanganyiko wa ambao uliua kisababishi magonjwa.[11] Ehrlich alikuwa ametuzwa Tuzo la Nobel mwaka 1908 kwa kazi yake kuhusu elimu ya kingamaradhi, na alianzisha matumizi ya madoa ili kuchunguza na kubaini bakteria, na kazi yake ilijikita kwenye misingi ya doa la Gram na doa la Ziehl-Neelsen.[12]

Mafanikio makubwa katika utafiti wa bakteria yalikuwa kutambuliwa kwa Carl Woese mwaka 1977 kwamba akea zilishuka kutokana na mabadiliko tofauti kutoka yale ya bakteria.[13] Uanishaji huu mpya wa jamii ya filojenetiki ulikitwa kwenye misingi ya kufululizwa kwa ribosomu RNA 16S, na ukagawa prokaryota katika makundi mawili yenye mageuko tofauti, kama mojawapo ya sehemu ya mifumo ya vikoa vitatu.[14]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Madigan M, Martinko J (editors) (2006). Brock Biology of Microorganisms (13th ed.). Pearson Education. p. 1096. ISBN 0-321-73551-X. 
  2. Porter JR (June 1976). "Antony van Leeuwenhoek: tercentenary of his discovery of bacteria". Bacteriological Reviews 40 (2): 260–9. PMC 413956. PMID 786250. 
  3. van Leeuwenhoek A (1684). "An abstract of a letter from Mr. Anthony Leevvenhoek at Delft, dated Sep. 17, 1683, Containing Some Microscopical Observations, about Animals in the Scurf of the Teeth, the Substance Call'd Worms in the Nose, the Cuticula Consisting of Scales". Philosophical Transactions (1683–1775) 14: 568–574. doi:10.1098/rstl.1684.0030. Retrieved 2007-08-19. [dead link]
  4. van Leeuwenhoek A (1700). "Part of a Letter from Mr Antony van Leeuwenhoek, concerning the Worms in Sheeps Livers, Gnats, and Animalcula in the Excrements of Frogs". Philosophical Transactions (1683–1775) 22: 509–518. doi:10.1098/rstl.1700.0013. Retrieved 2007-08-19. [dead link]
  5. van Leeuwenhoek A (1702). "Part of a Letter from Mr Antony van Leeuwenhoek, F. R. S. concerning Green Weeds Growing in Water, and Some Animalcula Found about Them". Philosophical Transactions (1683-1775) 23: 1304–11. doi:10.1098/rstl.1702.0042. Retrieved 2007-08-19. [dead link]
  6. Etymology of the word "bacteria". Online Etymology dictionary. Iliwekwa mnamo 2006-11-23.
  7. Pasteur's Papers on the Germ Theory. LSU Law Center's Medical and Public Health Law Site, Historic Public Health Articles. Iliwekwa mnamo 2006-11-23.
  8. The Nobel Prize in Physiology or Medicine 1905. Nobelprize.org. Iliwekwa mnamo 2006-11-22.
  9. O'Brien S, Goedert J (1996). "HIV causes AIDS: Koch's postulates fulfilled". Curr Opin Immunol 8 (5): 613–618. PMID 8902385. doi:10.1016/S0952-7915(96)80075-6. 
  10. Thurston A (2000). "Of blood, inflammation and gunshot wounds: the history of the control of sepsis". Aust N Z J Surg 70 (12): 855–61. PMID 11167573. doi:10.1046/j.1440-1622.2000.01983.x. 
  11. Schwartz R (2004). "Paul Ehrlich's magic bullets". N Engl J Med 350 (11): 1079–80. PMID 15014180. doi:10.1056/NEJMp048021. 
  12. Biography of Paul Ehrlich. Nobelprize.org. Iliwekwa mnamo 2006-11-26.
  13. Woese C, Fox G (1977). "Phylogenetic structure of the prokaryotic domain: the primary kingdoms". Proc Natl Acad Sci USA 74 (11): 5088–5090. PMC 432104. PMID 270744. doi:10.1073/pnas.74.11.5088. 
  14. Woese CR, Kandler O, Wheelis ML (June 1990). "Towards a natural system of organisms: proposal for the domains Archaea, Bacteria, and Eucarya". Proceedings of the National Academy of Sciences of the United States of America 87 (12): 4576–9. PMC 54159. PMID 2112744. doi:10.1073/pnas.87.12.4576. 

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mikrobiolojia kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.