Meinradi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Meinradi akiuawa.
Abasia ya Einsiedeln.

Meinradi (Ujerumani, 797 hivi - Einsiedeln, Uswisi, 861) alikuwa mmonaki padri wa utawa wa Wabenedikto ambaye alikwenda kuishi kama mkaapweke akifuata mifano ya Mababu wa jangwani[1].

Umaarufu wake ulipomvutia umati wa watu, alijitafutia mahali pa upweke mkubwa zaidi kati ya milima inayozunguka ziwa la Zurich. Hatimaye aliuawa na majambazi[2].

Alipofariki pakajengwa baadaye kidogo monasteri kubwa iliyotembelewa na watu wengi[3].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 21 Januari[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.