Matongo (Tarime)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kwa kata nyingine zenye jina hili, tazama Matongo.

Matongo ni kata ya Wilaya ya Tarime katika Mkoa wa Mara, Tanzania yenye postikodi namba 31412.

Kata ya Matongo inaundwa na vijiji vinne: Mjini Kati, Nyangoto, Nyabichune na Matongo.

Umbali kutoka Tarime Mjini hadi Matongo ni kilometa 30.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi wa kata walihesabiwa kuwa 34,678 [1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 19,176 waishio humo.[2]

Shughuli kubwa za kiuchumi ni uchimbaji wa madini, ufugaji na kilimo.

Maeneo ya kata hii ndiyo sehemu pekee katika wilaya ya Tarime ambapo madini ya dhahabu hupatikana kwa wingi. Mgodi wa Kampuni ya Acacia, North Mara, upo ndani ya kata hii.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Kata za Wilaya ya Tarime Vijijini - Mkoa wa Mara - Tanzania

Binagi * Bumera * Ganyange * Gorong'a * Gwitiryo * Itiryo * Kemambo * Kibasuka * Kiore * Komaswa * Kwihancha * Manga * Matongo * Mbogi * Muriba * Mwema * Nyakonga * Nyamwaga * Nyansincha * Nyanungu * Nyarero * Nyarokoba * Pemba * Regicheri * Sirari * Susuni


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Mara bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Matongo (Tarime) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Usiingize majina ya viongozi au maafisa wa sasa maana wanabadilika haraka mno.