Malaika Mikaeli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Malaika Mkuu Mikaeli)
Mchoro wa Kiorthodoksi wa karne ya 13 uliopo katika monasteri ya Mtakatifu Katerina kwenye Mlima Sinai.
Mchoro wa Guido Reni ukionyesha ushindi wa malaika mkuu Mikaeli dhidi ya Shetani, 1636.

Malaika Mikaeli (kwa Kiebrania מִיכָאֵל, Micha'el au Mîkhā'ēl, maana yake Nani kama Mungu; kwa Kigiriki Μιχαήλ, Mikhaḗl; kwa Kiarabu ميخائيل, Mīkhā'īl) anaheshimiwa kama malaika mkuu katika imani ya dini za Uyahudi, Ukristo na Uislamu.

Katika Biblia ya Kiebrania anatajwa mara tatu katika Kitabu cha Danieli.

Katika Agano Jipya la Biblia ya Kikristo anatajwa katika Waraka wa Yuda na katika Kitabu cha Ufunuo.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 29 Septemba[1][2]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Martyrologium Romanum
  2. Sikukuu ya Kianglikana huitwa “Michael na Malaika Wote” (kwa Kiingereza Michael and All Angels).

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.