Eneo la ng'ambo la Ufaransa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Maeneo ya ng'ambo ya Ufaransa ni maeneo nje ya Ulaya zilizokuwa koloni lakini zimeendelea kuwa sehemu za Ufaransa.

Hali ya kisheria[hariri | hariri chanzo]

Maeneo haya hutofautiana katika hali ya kisheria lakini wakazi wao wote ni raia wa Ufaransa na kila eneo linachagua wabunge wake kwa bunge la Paris. Isipokuwa maeneo yasiyokaliwa na watu hawana mbunge.

  • mengine ni mikoa (departement) kamili sawa na mikoa mingine ndani ya Ufaransa bara; maeneo yao ni sehemu ya Umoja wa Ulaya.
  • mengine ni jumuiya za kujitawala (collectivite) chini ya Ufaransa; hazihesabiwi kuwa sehemu za Umoja wa Ulaya; zinajitwala katika mambo ya ndani lakini mambo ya nje, jeshi na sheria huendeshwa na serikali ya kitaifa na sheria za bunge la Paris.
  • kuna bado eneo moja la ng'ambo linalotawaliwa na serikali ambalo ni visiwa vya kusini vya Kifaransa katika Bahari Hindi.

Mikoa ya Ng'ambo (Département d'outre-mer) au Jimbo la Ng'ambo (Région d'outre-mer)[hariri | hariri chanzo]

Eneo la Ng'ambo (Territoire d'outre-mer)[hariri | hariri chanzo]

Jumuiya za Kujitawala za Ng'ambo Collectivité d'outre-mer[hariri | hariri chanzo]

Jumuiya hizi zilianzishwa kwa mabadiliko ya katiba ya Ufaransa mwaka 2003. Kila jumuiya imeundwa kwa sheria ya pekee.

Nouvelle-Calédonie au Kaledonia Mpya[hariri | hariri chanzo]

  • Kaledonia Mpya (katika Pasifiki ya kusini) ni eneo la pekee; sehemu ya wakazi wanadai uhuru na kati ya 2014 na 2019 wakazi wote watapiga kura kuhusu swali la kubaki na Ufaransa au kuanzisha nchi huru.

Visiwa visivyokaliwa na watu[hariri | hariri chanzo]

Ufaransa hutawala au kudai utawala juu ya visiwa vidogovidogo bila wakazi:

Bahari Hindi[hariri | hariri chanzo]

Îles Éparses[hariri | hariri chanzo]

Visiwa hivi hudaiwa pia na Madagaska na Tromelin inadaiwa na Shelisheli.

Pasifiki[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]