Nenda kwa yaliyomo

Lugha za Kiturki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Lugha ya Kiturki)
Usambaji wa lugha za Kiturki katia Asia

Lugha za Kiturki ni kundi la lugha zaidi ya 30 zinazozungumzwa kutoka Ulaya ya Mashariki hadi Asia ya Kati na watu milioni 210. Zinahesabiwa kuwa sehemu za lugha za Kialtai pamoja na Kichina, Kimongolia, Kijapani na Kikorea. Wasemaji wa lugha za Kiturki husikizana kwa kiasi kikubwa. Lugha ya Kiturki inayojulikana zaidi kimataifa pia yenye wasemaji wengi ni Kituruki cha Uturuki.

Asili ya wasemaji wa lugha za Kiturki inadhaniwa kuwa sehemu za Mongolia. Kati ya karne za 6 hadi 10 walisambaa hadi Asia ya Magharibi na baada ya kutwaa Milki ya Bizanti waliingia pia katika Ulaya ya kusini-mashariki.

Lugha za Kiturki zenye wasemaji wengi

[hariri | hariri chanzo]

Lugha tatu kubwa za kundi hili ni

[hariri | hariri chanzo]

Lugha za Kiturki zenye wasemaji zaidi ya milioni moja:

[hariri | hariri chanzo]


Mifano ya maneno ya lugha za Kiturki

[hariri | hariri chanzo]

Mifano ifuatayo inaonyesha jinsi gani lugha za Kiturki zinavyofanana:

Kiswahili Kiturki
cha Kale
Kituruki Kiturkmeni Kitatari Kikazakhstan Kiuzbeki Kiuiguri
Mamaanaanne/anaeneanaanaonaana
puaburunburunburunborynmurınburunburun
mkonoqolkolqolkulqolqo'lkol
barabarajolyolýoljulzholyo'lyol
mnenesemizsemizsemizsimyzsemizsemizsemiz
ardhitopraqtopraktopraqtufraktopıraqtuproqtupraq
damuqankangankanqanqonqan
majivukülkülkülkölkülkulkül
majisuvsusuwsywsuwsuvsu
nyeupeaqakakakaqoqaq
nyeusiqarakaragarakaraqaraqoraqara
nyekunduqyzylkızılqyzylkyzylqızılqizilqizil
angakökgökgökkükkökko'kkök


Makala hii kuhusu "Lugha za Kiturki" inatumia neno au maneno ambayo si ya kawaida; matumizi yake ni jaribio kwa jambo linalotajwa.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao.

Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazina neno kwa jambo linalojadiliwa.