Kolo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Kata ya Kolo
Nchi Tanzania
Mkoa Dodoma
Wilaya Kondoa Mjini
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 5,649
Michoro ya kale karibu na Kolo

Kolo ni kata ya Wilaya ya Kondoa Mjini katika Mkoa wa Dodoma, Tanzania, yenye postikodi namba 41704[1].

Kolo iko kwenye barabara kuu kati ya Babati na Kondoa. Ndipo mahali pa kufikia kwa michoro ya Kondoa iliyo karibu na sehemu hiyo.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 5,649 [2]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 5,243 [3] waishio humo.

Baadhi ya vijiji vya kata ya Kolo vyenye shule ya msingi ni Kolo yenyewe, Bolisa, Gubali, Hachwi na Itiso. Asilimia kubwa za wakazi wa kata ya Kolo ni Warangi, ingawa zamani ilikuwa eneo la Waalagwa.

Shule ya msingi ya Kolo ni ya kwanza katika wilaya ya Kondoa. Ilifunguliwa mwaka wa 1917 chini ya utawala wa Sultani Salimu Kimolo ambaye ikulu yake bado ipo katika kijiji cha Kolo.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-03-21. Iliwekwa mnamo 2017-10-08. 
  2. https://www.nbs.go.tz
  3. "Sensa ya 2012, Dodoma - Kondoa DC". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2004-01-02. Iliwekwa mnamo 2016-05-18. 
Kata za Wilaya ya Kondoa Mjini - Mkoa wa Dodoma - Tanzania

Bolisa | Chemchem | Kilimani | Kingale | Kolo | Kondoa Mjini | Serya | Suruke


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Dodoma bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kolo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.