Kamili wa Lellis

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Kamilo wa Lellis)
Mt. Kamili wa Lellis, M.I., pamoja na mgonjwa.

Kamili wa Lellis (Bucchianico, wilaya ya Chieti, mkoa wa Abruzzo, leo nchini Italia, 25 Mei 1550 - Roma, 14 Julai 1614) alikuwa padri na mwanzilishi wa shirika la kitawa maalumu kwa ajili ya huduma za wagonjwa: Watumishi wa Wagonjwa, kwa kifupi M.I.

Kabla ya hapo alijiunga na jeshi bado kijana sana akaonekana kupenda anasa hadi alipoongoka na kujitosa kuhudumia waliolazwa katika hospitali ya wasiotibika kama kwamba ni Yesu mwenyewe[1].

Alitangazwa na Papa Benedikto XIV kuwa mwenye heri mwaka 1742, halafu mtakatifu mwaka 1746.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 14 Julai[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.