Jerlando wa Agrigento

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kanisa kuu la Agrigento.

Jerlando wa Agrigento (au Gerland wa Besançon; alifariki 25 Februari 1100) alikuwa askofu wa Kanisa Katoliki huko Agrigento, Sicilia, leo nchini Italia.

Alitangazwa mtakatifu mwaka 1159.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 25 Februari[1].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Inasadikika kwamba alizaliwa Besançon (Ufaransa), akiwa ndugu wa mfalme wa Kinormani Roger I wa Sisilia.

Baada ya huyo kufukuza Waarabu kutoka kisiwa cha Sisilia, mwaka 1088 (au 1093) alimuita Jerlando awe askofu wa Agrigento, wa kwanza baada ya utawala wa Kiislamu, ili arudishe Ukristo katika kisiwa chote.

Alifanya kazi hiyo kwa bidii na mafanikio makubwa hadi kifo chake, akiunda upya Kanisa, lililokuwa limebaki na waumini wachache tu wa Ukristo wa Mashariki, kuwa la Kilatini[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.