Isidori mkulima

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Isidori mkulima.
Mt. Isidro na Mt. Maria.

Isidori mkulima (kwa Kihispania San Isidro Labrador, Madrid, Castilia, 1070 hivi – Madrid, 15 Mei 1130[1]) alikuwa mkulima wa Hispania maarufu kwa upendo wake kwa maskini na wanyama.

Pamoja na mke wake, mwenye heri Maria wa Cabeza, aliwajibika katika kazi ngumu za shambani, akivuna kwa uvumilivu wake tuzo ya mbinguni kuliko mazao ya ardhi akawa kielelezo cha mkulima Mkristo.

Papa Paulo V alimtangaza mwenye heri tarehe 2 Mei 1619, halafu Papa Gregori XV alimtangaza mtakatifu tarehe 12 Machi 1622.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[2] .

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. ABC. Las idas y venidas del cuerpo incorrupto de San Isidro Labrador. Iliwekwa mnamo 21 November 2016.
  2. Roman Martyrology 2001 for 21st-century date; Catholic Encyclopedia (1910) for (same) early 20th-century date

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.