Gotardo wa Hildesheim

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Godehard wa Hildesheim)
Mt. Gotardo katika mavazi ya askofu, Hildesheim.

Gotardo wa Hildesheim, O.S.B. (jina asili: Gotthard au Godehard; Niederaltaich, Bavaria, 9604 Mei 1038) alikuwa mmonaki, padri, abati na hatimaye (2 Desemba 1022) askofu nchini Ujerumani[1].

Kama kiongozi wa wamonaki, alitembelea na kuanzisha monasteri mbalimbali. Halafu kama askofu alijitahidi kustawisha jimbo lake, akirudisha nidhamu kati ya wakleri na kuunda shule kadhaa.

Papa Innocent II alimtangaza mtakatifu mwaka 1131.

Sikukuu yake huadhimishwa na Wakatoliki na Waorthodoksi tarehe 5 Mei[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. www.santiebeati.it/dettaglio/51950
  2. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.