Gilbati wa Neuffonts

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake huko Bad Schussenried, Ujerumani.

Gilbati of Neuffonts, O. Praem. (Auvergne, leo nchini Ufaransa, mwishoni mwa karne ya 11 - Saint-Didier-la-Forêt, Ufaransa, 6 Juni 1152) alikuwa mkabaila aliyeishi kama mkaapweke kwa miaka michache kabla hajajiunga na shirika la Wakanoni wa Premontree, na kufanywa abati.

Kabla ya kutawa alikuwa na mke na binti mmoja akashiriki katika vita vya Msalaba (1146). Baada ya kukubaliana na mwenzake wa ndoa, alianzisha monasteri ya kike huko Aubeterre iliyoongozwa kwanza na mke wake, halafu na binti yao. Alianzisha pia hospitali kwa ajili ya wakoma na monasteri ya kiume huko Neufforts[1].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu. Papa Benedikto XIII alithibitisha heshima hiyo tarehe 22 Januari 1728.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 6 Juni[2]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Jean-Claude Souliac, Gilbert, saint patron du Bourbonnais, Charroux, Éditions des Cahiers bourbonnais, 1996.
  • Jean-Claude Souliac, Bulletin historique et scientifique de l'Auvergne, 1933.
  • Rosa Giorgi, Le petit livre des saints, Paris, Larousse, 2006, p. 340. ISBN|2-03-582665-9
  • Johann Samuel Ersch, Johann Gottfried Gruber u. a.: Gilbert der Heilige. In: Allgemeine Encyklopadie der Wissenschaften und Kunste. Section 1, Theil 67. Brockhaus, Leipzig 1858, S. 200.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.