Emerensyana wa Roma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtakatifu Emerensyana akiuawa.

Emerensyana wa Roma (alifariki Roma, Italia, 304 hivi) alikuwa na undugu[1][2] na Agnes wa Roma, bikira mwenye umri wa miaka 12 ambaye alikataa kuolewa kwa sababu ya imani yake ya Kikristo na kwa sababu hiyo aliteswa akauawa wakati wa dhuluma ya Dola la Roma dhidi ya Wakristo.

Siku chache baadaye, Emerensyana, ambaye alikuwa anajiandaa kubatizwa, alikwenda kwenye kaburi la Agnes, kumbe alishambuliwa na kuuawa kwa mawe na umati wa Wapagani.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 23 Januari[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.