Egidi Maria wa Mt. Yosefu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Ejidi wa Mt. Yosefu)
Sanamu yake iliyotengenezwa kwa karatasi iliyopondwa mwaka 1920.

Egidi Maria wa Mt.Yosefu (Taranto, 16 Novemba 1729 - Napoli 7 Februari 1812), alikuwa mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo Pekupeku kutoka Italia kusini.

Kila siku alikuwa akiombaomba kwa unyenyekevu msaada katika mitaa ya mji akirudisha maneno ya faraja kwa wote.

Jina lake la awali lilikuwa Francesco Antonio Domenico Pasquale Pontillo.

Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu tangu alipotangazwa na Papa Yohane Paulo II mwaka 1996. Kabla ya hapo alitangazwa mwenye heri na Papa Leo XIII mwaka 1888.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[1].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.