Bamba la Afrika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bamba la Afrika (nyekundu-njano) kati ya mabamba gandunia ya dunia yetu
Ramani ya Afrika ya Mashariki inayoonyesha volkeno kadhaa (pembetatu nyekundu) na pembetatu ya Afar - eneo la kuachana kwa bamba la Uarabuni na bamba la Afrika linalopasuka hapa kuwa bamba la Afrika ya Kinubia na la Afrika ya Kisomalia.

Bamba la Afrika ni kati ya mabamba makubwa ya gandunia ya dunia yetu. Lipo chini ya bara la Afrika na chini ya sehemu za bahari zinazopakana nalo yaani tako la bara[1].

Bamba hilo limepakana na bamba la Ulaya-Asia, bamba la Uarabuni, bamba la Uhindi, bamba la Australia, bamba la Antaktika na bamba la Amerika ya Kaskazini. Inawezekana ya kwamba limepakana na mabamba madogo mengine yasiyojulikana bado.

Bamba la Afrika lina mwendo wa kuelekea kaskazini unaopimwa kuwa sm 2.15 kwa mwaka[2]. Kwa mkasi huo bara la Afrika litagusana na Hispania ya Kusini baada ya miaka 650,000 na kufunga mlango wa bahari wa Gibraltar na hivyo kuifanya Mediteranea kuwa ziwa.

Bamba la Afrika lenyewe liko katika mwendo wa kupasuka kwenye mstari wa ufa la Afrika ya Mashariki kutoka Eritrea kupitia Ethiopia, Kenya, Tanzania, Malawi na mwishowe katika Msumbiji. Sehemu hizo mbili za bamba la Afrika huitwa na wataalamu bamba la Afrika ya Kinubia na la Afrika ya kisomalia[3].

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hiyo kuhusu "Bamba la Afrika" inatumia neno ambalo si kawaida na matumizi yake ni jaribio kwa jambo linalotajwa.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao.

Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazina neno kwa jambo linalojadiliwa.

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bamba la Afrika kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.