Bamba la Antaktiki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Bamba la Antaktika)
Bamba la Antaktiki

Bamba la Antaktiki ni bamba la gandunia linalobeba bara la Antaktiki na sehemu za sakafu ya bahari jirani.

Bamba hilo huwa na eneo la Km² 60,900,000.

Mabamba yanayopakana ni Bamba la Nazca, Bamba la Amerika ya Kusini, Bamba la Afrika, Bamba la Australia na Bamba la Pasifiki.

Kihistoria baada ya kuvunjika kwa Gondwana (sehemu ya kusini ya bara kuu la kale Pangaia, bamba la Antaktiki lilianza kusogea pale lilipo, kwenye ncha ya kusini ya dunia, na hivyo kusababisha tabianchi baridi kabisa ya Antaktiki. [1]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Fitzgerald, Paul (2002). "Tectonics and landscape evolution of the Antarctic plate since the breakup of Gondwana, with an emphasis on the West Antarctic Rift System and the Transantarctic Mountains". Royal Society of New Zealand Bulletin (35): 453–469. Iliwekwa mnamo February 1, 2015.  Check date values in: |accessdate= (help)