Atenodori

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Gregori Mtendamiujiza, kaka wa Atenodori, alivyochorwa katika karne ya 14.

Atenodori (Kaisarea Mpya, 215 hivi – Kaisarea Mpya, Ponto, leo nchini Uturuki, 270 hivi) alikuwa askofu wa karne ya 3.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 7 Novemba[1].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Atenodori alikuwa mdogo wa Gregori Mtendamiujiza. Familia yao ilikuwa haijaingia dini hiyo, ambayo yeye alikuja kuifahamu akiwa na umri wa miaka 12, baada ya kufiwa baba yake.

Pamoja na kaka yake, Atenodori alikuwa ametumwa Beirut (leo nchini Lebanon) kwa ajili ya masomo ya sheria; kutoka huko walisafiri hadi Kaisarea ya Palestina. Huko walisikia habari za msomi maarufu Origen, mkuu wa Chuo cha Katekesi cha Aleksandria, aliyekuwa anaishi huko. Udadisi uliwafanya wakamsikilize na kuongea naye; ndipo walipovutiwa sana, kiasi cha kusahau kabisa Beirut na sheria.

Umaarufu alioupata kwa ujuzi wake wa Biblia uliofanya apewe daraja takatifu hiyo akiwa bado kijana (260 hivi) [2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/76380
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.