Ansfridi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya Mt. Ansfridi huko Huy.

Ansfridi (Ubelgiji, 940 hivi – Leusden, leo nchini Uholanzi, 3 Mei 1010) alikuwa mtawala wa Huy, maarufu kwa maadili ya Kikristo pamoja na mke wake na binti yao pekee.

Alipofiwa mke wake, alitaka kujiunga na monasteri, lakini kaisari Oto III alimfanya askofu mkuu wa Utrecht mwaka 955 akaongoza jimbo hilo hadi kifo chake, ingawa alipozidi kudhoofika kutokana na malipizi yake akawa mmonaki kama alivyotamani kama moja ya monasteri alizozianzisha [1][2].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa katika tarehe 3 Mei[3].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.