Mitholojia ya Kigiriki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Kichwa cha Sanamu ya Zeu

Mitholojia ya Kigiriki ni ukusanyaji wa masimulizi na hadithi za Ugiriki ya Kale, kuhusu miungu na mashujaa wao. Zilikuwa moja ya sehemu ya dini ya Ugiriki ya Kale.

Yaliyomo

Miungu Kumi na Miwili ya Olimpos [hariri]

Jina la Kigiriki Jina la Kiswahili Maelezo
Aφροδίτη (Afrodítē) Afrodita Mungu wa kike wa upendo na uzuri.
Aπόλλων (Apóllōn) Apolo Mungu wa nuru na ushairi.
Άρης (Árēs) Ares Mungu wa vita.
Άρτεμις (Ártemis) Artemi Mungu wa kike wa uwindo.
Αθηνά (Athēná) Athena Mungu wa kike wa elimu na hekima.
Δημήτηρ (Dēmḗtēr)

Δήμητρα (Dḗmētra)

Demetra Mungu wa kike wa mimea na kilimo.
Διόνυσος (Diónysos) Dioniso Mungu wa divai.
Έρως (Érōs) Ero Mungu wa mapenzi.
ᾍδης (Ádēs) Hade Mungu wa kuzimu na bwana wa waliokufa.
Ήφαιστος (Ḗfaistos) Hefaisto Mungu wa uhunzi.
Ήρα (Ḗra) Hera Mungu wa kike wa ndoa na malkia ya miungu.
Ερμής (Ermḗs) Herme Mjumbe wa miungu.
Ἑστία (Estía) Hestia Mungu wa kike wa moto.
Ποσειδῶν (Poseidṓn)

Ποσειδώνας (Poseidṓnas)

Poseidoni Mungu wa bahari.
Ζεύς (Zeús)

Δίας (Días)

Zeu Mungu wa radi na mfalme wa miungu.

Protogenoi [hariri]

Jina la Kigiriki Jina la Kiswahili Maelezo
Αιθήρ (Aithḗr) Aitheri Mungu wa anga.
Ἀνάγκη (Anágkē) Ananka Mungu wa kike wa lazima.
Έρεβος (Érevos) Erebo Mungu wa giza.
Γαία (Gaía) Gaya Mungu wa kike wa ardhi.
Ημέρα (Ēméra) Hemera Mungu wa kike wa mchana.
Χάος (Kháos) Khaos
Χρόνος (Khrónos) Khrono Mungu wa muda.
αἱ Nῆσοι (ai Nḗsoi) Visiwa Miungu ya kike ya visiwa.
Νύξ (Nýx) Niksi Mungu wa kike wa usiku.
Ουρανός (Ouranós) Urano Mungu wa mbingu.
Ούρος (Oúros) Milima Miungu ya milima.
Πόντος (Póntos) Ponto Mungu wa bahari ya dunia nzima.
Τάρταρος (Tártaros) Tartaro Mungu wa tartaro.
Θάλασσα (Thálassa) Thalasa Malkia wa bahari na mke wa Ponto.

Titani Kumi na Wawili [hariri]

Jina la Kigiriki Jina la Kiswahili Maelezo
Ὑπερίων (Yperíōn) Hiperioni Mungu wa nuru ya jua.
Ἰαπετός (Iapetós) Yapeto
Κοῖος (Koïos) Koyo Mungu wa fahamu.
Κρεῖος (Kreïos) Kreyo
Κρόνος (Krónos) Krono Mfalme wa Titani.
Mνημοσύνη (Mnēmosýnē) Mnemosina Mungu wa kike wa kumbukumbu.
Ὠκεανός (Ōkeanós) Okeano Mungu wa bahari kuu.
Φοίβη (Foívē) Foiba
Ῥέα (Réa) Rea Malkia wa Titani na mke wa Krono.
Τηθύς (Tēthýs) Tethi Mungu wa kike wa mito.
Θεία (Theía) Theya Mungu wa kike wa uonaji.
Θέμις (Thémis) Themi

Majitu [hariri]

  • Hekatonkheire (Ἑκατόγχειρες) — majitu yenye mikono mia na miungu wa dhoruba na vimbunga.
    • Briareo (Βριάρεως)
    • Coto (Κόττος)
    • Gige (Γύγης)
  • Siklopsi (Κύκλωψ) - majitu-chongo watatu.
    • Arge (Ἄργης)
    • Bronte(Βρόντης)
    • Sterope (Στερόπης)

Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.