Ushairi
Kutoka Wikipedia
Ushairi ni utungo wa kisanaa ulio na madhumuni ya kutumbuiza au kuelimisha. Tena, ushairi ni tawi moja la fasihi andishi. Kinyume chake ni nathari.
Inawezekana kutunga mashairi yenyewe au kutumia lugha ya kishairi katika aina nyingine za kisanaa, kwa mfano tamthiliya au nyimbo.
Ushairi una historia ndefu. Kwa mfano, mwanafalsafa Aristotle katika kitabu chake Ushairi ("Poetics" kwa Kiingereza) anachunguza matumizi yake katika hotuba, tamthiliya, nyimbo na futuhi.
[hariri] Marejeo
Wamitila, K.W. 2003. Kamusi ya Fasihi: Istilahi na Nadharia, Nairobi: Focus Books.
| Makala hiyo kuhusu "Ushairi" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri". Ikiwepo makala kuhusu Ushairi kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili. |

