Lionel Messi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Lionel Messi (2018).
Messi akiangalia goli lake dhidi ya Iran.
Messi akiwa mazoezini 2014

Lionel Andrés Messi, (matamshi ya Kihispania: [ljonel andɾes mesi]; alizaliwa 24 Juni 1987) ni mchezaji wa mpira wa miguu wa Argentina anayecheza katika klabu ya Paris Saint-Germain F.C. (PSG) iliyopo nchini Ufaransa na timu ya taifa ya Argentina.

Mara nyingi huchukuliwa kuwa mchezaji bora wa nyakati zote, Messi kafanikiwa kuchukua tuzo za Ballon d’Or mara tano, kati ya hizo alichukua nne mfululizo, na rekodi ya kunyakua viatu vya dhahabu vya Ulaya mara sita. Maisha yake yote ya soka la kiushindani ameichezea klabu ya Barcelona.[1][2]

Ameshinda mataji 34 yakijumuisha kumi ya La Liga, [[manne ya UEFA Champions League na sita ya Copas del Rey, akiwa mfungaji machachari na kiungo mbunifu, Messi ana Rekodi ya magoli mengi aliyofunga katika La Liga (419), misimu katika soka la ulaya (50) na idadi kubwa ya bao tatu kwa mpigo katika UEFA (8) na idadi kubwa ya pasi za mwisho La Liga (169) na copa America (12). Kwa ujumla kafunga jumla ya magoli 698 katika maisha yake ya kiuchezaji ndani ya klabu na timu ya taifa.[3][4]

Akiwa mzaliwa kutoka katikati ya Argentina, Messi alipata ugonjwa wa homoni ya kukua akiwa mtoto. Alipokuwa na umri wa miaka 13, alihamia Hispania kujiunga na Barcelona, ambao walikubali kulipa matibabu yake. Baada ya mafanikio ya haraka kwenye timu ya watoto ya Barcelona, Messi alicheza mchezo wake wa kwanza wa kiushindani akliwa na umri wa miaka 17 mnamo Oktoba 2004. [5]

Licha ya kuwa katika hatari ya kujeruhiwa wakati wa michezo yake ya awali, alifanikiwa kujijenga kuwa mchezaji muhimu kwa klabu ndani ya miaka mitatu iliyofuata na kufanikiwa kutwaa taji la Ballon d’Or na mchezaji bora wa mwaka wa FIFA wa 2007, na alirudia mwaka uliofuata. Msimu wake wa kwanza bila vikwazo ni wa 2008-2009, ambapo aliisaidia Barcelona kunyakua mataji matatu kwa mpigo katika soka la Hispania.

Akiwa na umri wa miaka 22, Messi alishinda Ballon d'Or na tuzo ya Mchezaji bora wa Mwaka ya FIFA. Misimu mitatu ya mafanikio ilifuatia, Messi akishinda tuzo za FIFA Ballons d'Or mara tautu mfululizo, ikiwa ni pamoja na ya nne ambayo haikukabidhishwa. Katika msimu wa 2011-2012, aliweka rekodi kwenye La Liga kuwa mchezaji aliyefunga magoli mengi zaidi ndani ya msimu mmoja, Mnamo Machi 2012 alijitangaza kama mfungaji bora wa wakati wote wa Barcelona.

Kwa misimu miwili iliyofuata, alishika nafasi ya pili kwenye kuwania tuzo za Ballon d’Or nyuma ya mshindani wake mkubwa Cristiano Ronaldo. Messi alirudi kwenye kiwango cha juu msimu wa 2014-2015, na kuvunja rekodi ya magoli mengi kwa msimu mmoja ndani ya La Liga na ligi ya mabingwa ulaya UEFA mwezi Novemba 2014.

Kama mchezaji wa timu ya taifa ya Argentina, Messi anashikilia rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wowote wa Argentina. Mwaka 2005, alinyanyua kombe la FIFA mashindano ya vijana, akipata tuzo ya mchezaji bora na mfungaji bora pia, alipata medali ya dhahabu katika mashindano ya olimpiki yam waka 2008. Aina ya uchezaji, kukokota mipira na matumizi ya mguu wa kushoto kulipelekea wengi kumfananisha na mtangulizi wake Diego Maradona, ambaye alimtangaza Messi kuwa mrithi wake. Mchezo wake wa kwanza katika timu ya taifa mnamo Agosti 2005, ulimfanya Messi kuwa mchezaji mdogo zaidi wa Argentina kuwahi kucheza katika mashindano ya Kombe la Dunia ya FIFA katika toleo la 2006, na alifika fainali za Copa América mwaka 2007, ambapo alitwaa tuzo ya mchezaji mdogo wa mashindano hayo. Kama nahodha wa timu ya taifa kutoka Agosti 2011, aliiongoza Argentina kwenye mashindano matatu mfululizo; Kombe la Dunia la mwaka 2014, ambalo alishinda tuzo ya mchezaji bora na Copa América ya mwaka 2015 na 2016. Alitangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa mwaka 2016 lakini alibadili maamuzi hayo na kusaidia taifa lake kwenye mashindano ya kombe la dunia la FIFA 2018 na kushika nafasi ya tatu katika copa Anmerica ya 2019.

Kulingana na shirika la mpira la Ufaransa, Messi alitajwa kama mchezaji soka anayelipwa ghali Zaidi mwa miaka mitano kati ya sita kuanzia mwaka 2009 hadi 2014, na alitajwa kama mwanamichezo anayelipwa ghali Zaidi na jarida la forbes kwa mwaka 2019. Alikua miongoni mwa watu 100 wenye ushawishi zaidi kwa miaka ya 2011 na 2012. Messi anafadhiliwa na kampuni ya Adidas inayotengeneza vifaa vya michezo kuanzaia mwaka 2006.

Maisha ya awali[hariri | hariri chanzo]

Lionel Andrés Messi alizaliwa tarehe 24 Juni 1987 huko Rosario, ni wa tatu kati ya watoto wanne wa bwana Jorge Messi, meneja wa kiwanda cha chuma, na mkewe wake Celia Cuccittini, ambaye alifanya kazi katika viwanda vya sumaku. Kwa upande wa baba yake, yeye ni wa asili ya Italia na Hispania, mjukuu wa wahamiaji kutoka Marche na Catalonia, na kwa upande wa mama yake, ana asili ya Italia. Kukulia katika familia yenye mapenzi makubwa sana na soka, "Leo" alijenga mapenzi ya mchezo huo ntangu umri mdogo, alicheza mara kwa mara na kaka zake wakubwa, Rodrigo na Matías, na binamu zake, Maximiliano na Emanuel Biancucchi, ambao kwa sasa wanacheza mpira wa kulipwa. [6][7]

Alipokuwa na umri wa miaka minne alijiunga na klabu ya Grandoli, ambapo baba yake mzazi ndie aliyekua mkufunzi wake, ingawa mvuto wake wa kwanza kama mchezaji ulikuja kutoka kwa bibi yake, Celia, ambaye aliongozana naye kwenye mazoezi na mechi. Aliathirika sana na kifo chake kilichotokea muda mfupi kabla ya sherehe ya kuzaliwa kwake akiwa anatimiza umri wa miaka kumi na moja; tangu wakati huo, kama mkatoliki mwenye kujitolea, amekua akishangilia magoli anyofunga kwa kutazama na kuelezea vidole angani kama ishara ya kumuenzi bibi yake.[8]

"Wakati ulipomwona ungefikiri: mtoto huyu hawezi kucheza mpira, yeye ni mdogo, yeye ni tete sana, mdogo sana. Lakini mara moja utajua kwamba alizaliwa tofauti, kwamba alikuwa ni jambo la ajabu na kwamba alikuwa akienda kuwa kitu cha kushangaza." -Newell's Old Boys kocha wa kijana Adrián Coria anahisi hisia yake ya kwanza ya Messi mwenye umri wa miaka 12.[9]

Kama msaidizi mkuu wa Newell's Old Boys, Messi alijiunga na klabu ya Rosario akiwa na umri wa miaka sita. Katika kipindi cha miaka sita aliyoichezea Newell's, aliifungia magoli takribani 500 akiwa kama mwanachama wa "Machine ya '87", vijana wa timu hii ambayo ilicheza michezo mingi bila kupoteza walijipa jina kulingana na mwaka wao wa kuzaliwa, mara kwa mara walikua wakifanya maonyesho kwa kuchezea mipira (freestyle) katika michezo mikubwa wakati wa mapunziko. [10]

Maisha yake ya baadaye kama mchezaji wa kimataifa yalitishiwa wakati, akiwa na umri wa miaka 10, alipata ugonjwa wa homoni ya kukua. Bima ya afya ya baba yake ililipia matibabu kwa miaka miwili tu matibabu hayo yaligharimu kiasi cha dola za kimarekani $ 1,000 kwa mwezi, Newell ilikubali kuchangia, lakini baadaye ikatengua tena ahadi zao. Klabu ya Buenos Aires River Plate ilimchukua kutokana na pendekezo la, Pablo Aimar, lakini pia hawakuweza kulipa matibabu yake kutokana na anguko la kiuchumi nchini humo. [11]

Kwa sababu familia ya Messi ilikuwa na jamaa huko Catalonia, walijaribu kupanga Messi apate jaribio na klabu ya Barcelona mnamo Septemba 2000. Mkurugenzi wa timu ya kwanza Charly Rexach alitaka kumsajili mara moja, lakini bodi ya wakurugenzi ilikataa; wakati huo ilikuwa si kawaida kwa klabu za Ulaya kusaini wachezaji wa kigeni wa umri mdogo. Mnamo tarehe 14 Desemba, hatimaye Barcelona ilitoa msimamo wake na kukubali usajili wa Messi, na Rexach, bila karatasi nyingine iliyopo, alitoa mkataba juu ya leso. Mnamo Februari 2001, familia yake Messi ilihamia Barcelona, ambapo walipata makazi katika ghorofa moja karibu na uwanja wa klabu, Camp Nou. [12]

Katika mwaka wake wa kwanza nchini Hispania, Messi mara chache alicheza na Infantiles kutokana na mgogoro wa uhamisho na klabu yake ya awali ya Newell's; akiwa mgeni, alicheza katika mechi za kirafiki tu na mashindano ya katalani. Bila mpira, alijitahidi alipata tabu kujumuika na wachezaji wenzake, alikuwa na utulivu kiasi kwamba wenzake waliamini kuwa alikuwa bubu. Alipata sonona baada ya mama yake kurudi Rosario pamoja na ndugu zake na dada mdogo, María Sol, nay eye kubaki na baba yake Barcelona. [13][14]

Baada ya mwaka akiwa katika shule ya michezo ya Barcelona, La Masia, Messi hatimaye alijiunga na Shirikisho la Soka la Soka la Kihispania (RFEF) mnamo Februari 2002. Sasa aliweza kucheza katika mashindano yote, alianza kujenga urafiki na wachezaji wenzake, kati yao walikuwa Cesc Fàbregas na Gerard Piqué.[15]

Alikamilisha tiba yake ya ukuaji wa homoni akiwa na umri wa umri wa miaka 14, Messi akawa sehemu muhimu ya "Timu ya Baby Dream", moja ya timu ya vijana ya Barcelona iliyopata mafanikio sana. Katika msimu wake wa kwanza kamili (2002-03), alikuwa mchezaji bora akiwa na idadi ya bao 36 katika michezo 30 ya Cadet A, ambaye alishinda vikombe vitatu kwa mpigo vikijumuisha kombe la ligi na vikombe vya Hispania na Kikatalani. Mchezo wa fainali wa Copa Catalunya, waliopata ushindi wa 4-1 dhidi ya Espanyol ulisababisha wajulikane kama partido de la máscara. [16]

Wiki moja baada ya kupata jeraha la taya, Messi aliruhusiwa kuanza mchezo akiwa amevaa kifaa maalum cha kumkinga; kifaa hicho kilimbughudhi na aliamua kukitoa, alifunga magoli mawili kabla ya kupumzishwa dakika kumi baadaye, kuelekea mwishoni mwa msimu, alipata ofa ya kujiunga na Arsenal, ikiwa ofa ya kwanza kutoka klabu ya kigeni, lakini wakati Frabregas na Piqué waliondoka kuelekea England, yeye aliamua kubaki Barcelona.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Lionel Messi kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.