Gottfried Leibniz
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
| Gottfried Wilhelm von Leibniz |
|
|---|---|
|
|
|
| Alizaliwa | 1 Julai 1646 Leipzig |
| Alikufa | 14 Novemba 1716 Hannover |
| Nchi | Ujerumani |
| Kazi yake | balozi na mtaalamu wa falsafa, hisabati, historia na sheria |
Gottfried Wilhelm Leibniz (pia Leibnitz au von Leibniz) alikuwa mwanasayansi na mwanafalsafa Mjerumani aliyeandika hasa kwa Kilatini na Kifaransa.
Anasemekana alikuwa mtu wa mwisho aliyeweza kushika ujuzi wote wa ustaarabu wake.
Alisoma mwenyewe sharia na falsafa. Akahudumia familia mbili za kitemi nchini Ujerumani, kwanza katika Bavaria na baadaye katika Hannover. Katika utumishi wa watemi hao alisafiri kote Ulaya kama mbalozi wao. Sehemu ya mwisho wa maisha yakke alikaa Hannover alipounda maktaba kubwa.
Alibuni hisabati ya kalkulasi na pia hisabati ya binari ambayo ni msingi wa teknolojia ya kompyuta. Alitengeneza pia mashine ya mahesabu.
Katika falsafa alitoa jibu la swali la theodisea au jinsi gani Mungu mwenye haki anaweza kuruhusu mabaya. Alisema ya kwamba dunia yetu jinsi ilivyo si baya lakini ni dunia bora iliyoweza kuumbwa na Mungu.
Alishughulika mambo mengi sana pamoja na