Nyambizi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nyambizi Alvin (1978) ni chombo cha kisayansi kinachochunguza vilindi vya bahari.
Nyambizi ya Marekani "USS Sea Owl" wakati wa vita kuu ya pili ya dunia.

Nyambizi (pia: sabmarini kutoka Kiingereza submarine) ni meli na mara nyingi manowari inayosafiri chini ya maji.

Kuna pia nyambizi zenye shabaha za kisayansi au kibiashara.

Matumizi ya kivita yalianzishwa hasa na Ujerumani wakati wa vita kuu za dunia.

Tangu miaka ya 1950 nchi nyingi kama Ufaransa, Marekani na Urusi zina nyambizi za pekee ambazo huendeshwa kwa injini za kinyuklia zenye uwezo wa kuzunguka dunia yote chini ya maji. Mara nyingi hubeba makombora ya kinyuklia.

Makala hii kuhusu mambo ya teknolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hiyo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.