Yohane wa Mungu
Jump to navigation
Jump to search
Mtakatifu Yohane wa Mungu (8 Machi 1495 – 8 Machi 1550) alikuwa mtawa wa Ureno alitoa huduma zake nchini Hispania.
Ametambuliwa na Kanisa Katoliki kuwa mtakatifu.
Sikukuu yake ni tarehe 8 Machi[1].
Maisha[hariri | hariri chanzo]
Yohane wa Mungu alizaliwa nchini Ureno mwaka 1495.
Baada ya kuishi maisha ya hatari kama askari, na akitamani kutumia maisha yake yaliyokuwa yamebaki kwa kufanya matendo mema, alijitoa mhanga kabisa ili awauguze wagonjwa.
Alianzisha hospitali huko Granada nchini Hispania, na yeye pamoja na wafuasi wake wakaunda Shirika la Wauguzi la Mt. Yohane wa Mungu.
Alijulikana sana kwa upendo wake kwa wagonjwa na maskini.
Alikufa siku ya kufikisha umri wa miaka 55 kamili, tarehe 8 Machi, mwaka 1550 huko Granada.
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
- The Life of St. John of God
- John of God at the Catholic Encyclopedia
- Founder Statue in St Peter's Basilica
- Order of Knights of Saint John of God
- St. John of God Hospital Sierra Leone Archived Juni 25, 2013 at the Wayback Machine.
- St. John of God in The Netherlands
![]() |
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |