Yohane wa Mungu
Mandhari

Yohane wa Mungu (8 Machi 1495 – 8 Machi 1550) alikuwa mtawa wa Ureno aliyetoa huduma zake nchini Hispania.
Ametambuliwa na Kanisa Katoliki kuwa mtakatifu.
Maisha
[hariri | hariri chanzo]Yohane wa Mungu alizaliwa nchini Ureno mwaka 1495.
Baada ya kuishi maisha ya hatari kama askari, na akitamani kutumia muda wake uliokuwa umebaki kwa kufanya matendo mema, alijitoa mhanga kabisa ili awauguze wagonjwa na maskini kwa upendo usiokubali uchovu [2].
Kwa ajili hiyo alianzisha hospitali huko Granada nchini Hispania, akapokea wafuasi ambao baadaye waliunda Shirika la Wauguzi la Mt. Yohane wa Mungu [3].
Alijulikana sana kwa upendo wake kwa wagonjwa na maskini.
Alifariki huko Granada siku ya kutimiza umri wa miaka 55, tarehe 8 Machi, mwaka 1550.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Martyrologium Romanum
- ↑ Sehemu ya barua yake mojawapo imetafsiriwa kwa Kiswahili katika Masomo ya Breviari - Sikukuu za Bwana, za Bikira Maria na za Watakatifu - Ndanda Mission Press 1978, uk 83-85.
- ↑ https://www.santiebeati.it/dettaglio/26300
Marejeo ya Kiswahili
[hariri | hariri chanzo]- John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 84-85
- Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 69
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- The Life of St. John of God Ilihifadhiwa 7 Machi 2016 kwenye Wayback Machine.
- John of God at the Catholic Encyclopedia
- Founder Statue in St Peter's Basilica
- Order of Knights of Saint John of God
- St. John of God Hospital Sierra Leone Ilihifadhiwa 25 Juni 2013 kwenye Wayback Machine.
- St. John of God in The Netherlands
| Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |
