Yohane wa Mungu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Yohane wa Mungu
Sanamu ya Mtakatifu Yohane wa Mungu katika Vilar de Frades, Barcelos, Ureno.

Yohane wa Mungu (8 Machi 14958 Machi 1550) alikuwa mtawa wa Ureno aliyetoa huduma zake nchini Hispania.

Ametambuliwa na Kanisa Katoliki kuwa mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 8 Machi[1].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Yohane wa Mungu alizaliwa nchini Ureno mwaka 1495.

Baada ya kuishi maisha ya hatari kama askari, na akitamani kutumia muda wake uliokuwa umebaki kwa kufanya matendo mema, alijitoa mhanga kabisa ili awauguze wagonjwa na maskini kwa upendo usiokubali uchovu.

Kwa ajili hiyo alianzisha hospitali huko Granada nchini Hispania, akapokea wafuasi ambao baadaye waliunda Shirika la Wauguzi la Mt. Yohane wa Mungu.

Alijulikana sana kwa upendo wake kwa wagonjwa na maskini.

Alifariki huko Granada siku ya kutimiza umri wa miaka 55, tarehe 8 Machi, mwaka 1550.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.