Wiliamu wa Vercelli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu yake katika basilika la Mt. Petro, Vatikano.

Wiliamu wa Vercelli, O.S.B. (Vercelli, Piemonte, 1085 - Sant'Angelo dei Lombardi, Campania, 25 Juni 1142) alikuwa abati nchini Italia na mwanzilishi wa urekebisho wa Wabenedikto wa Monte Vergine ambao aliueneza sehemu mbalimbali kwa wanaume na kwa wanawake [1][2].

Bado kijana alijifanya fukara kwa ajili ya Kristo na kuhama mkoa wake akihiji huko na huko hadi Yohane wa Matera alipomhimiza kuanzisha monasteri alipolea wafuasi wake kwa mafundisho bora ya kiroho[3].

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila tarehe 25 Juni[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.