Wiliamu Pinchon

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kaburi lake katika kanisa kuu la Saint-Brieuc.

Wiliamu Pinchon (Saint-Alban, 1180 - Saint-Brieuc, 1234) alikuwa askofu wa Saint-Brieuc, Bretagne, Ufaransa, maarufu kwa wema na unyofu.

Alijenga kanisa kuu la jimbo lake.

Katika kutetea waumini wake na haki za Kanisa, alidhulumiwa sana na kupelekwa uhamishoni, akavumilia yote kwa utulivu [1].

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 29 Julai[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • A. Barthelémy, Ancien évêques de Bretagne. Histoire et monuments. Diosèse de Saint-Brieuc, Tome III, Paris, Saint Brieuc, 1864.
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.