Wakristo wa Kiyahudi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Tohara ya Yesu ilivyoonyeshwa kwa kuchonga marumaru, kanisa kuu la Chartres, Ufaransa.

Wakristo wa Kiyahudi walikuwa Wayahudi waliomuamini Yesu kuwa ndiye Masiya (Kristo) aliyetabiriwa katika dini yao.[1]

Mwanzoni Kanisa la wafuasi wa Yesu liliundwa na watu wa namna hiyo karibu peke yao, lakini kadiri miaka ya karne ya 1 ilivyozidi kwenda, waamini kutoka mataifa mengine waliongezeka hadi kuwazidi hao wenye asili ya Kiyahudi.

Hatimaye Wakristo wa Kiyahudi walionekana kundi dogo la watu waliozidi kuzingatia mno mambo ya Agano la Kale, tofauti na Wakristo wenzao[2][3]; kwa mfano: tohara, Sabato na ibada za sinagogini[1][4][5].[6] Tofauti kati yao na Wayahudi wengine ilikuwa tu imani kuhusu Yesu.[7]

Baadhi yao walisisitiza umuhimu wa desturi za Kiyahudi kiasi cha kudai hata Wakristo wenye asili ya mataifa wazifuate[8], lakini Mtaguso wa Yerusalemu (Mdo 15:6-35) uliamua tofauti[8], wakaendelea kumpinga Mtume Paulo na kuvuruga kazi yake ya uinjilishaji wa mataifa.

Wakristo wa Kiyahudi walidhoofisha sana na Vita vya Wayahudi kwa ajili ya kujikomboa (66-135), na maangamizi ya Hekalu la Yerusalemu (70) pamoja na itikadi kali ambayo iliongoza Uyahudi baadaye na kufukuza Wakristo wote kutoka sinagogini.

Hatimaye hata Kanisa la Yerusalemu lilibaki mikononi mwa Wakristo wasio Wayahudi kwa asili.

Pamoja na hayo, mwelekeo wa kutaka Wakristo wafuate masharti mengi au hata yote ya Torati umeendelea hadi leo katika madhehebu mbalimbali.[8]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 David Noel Freedman, Allen C. Myers (2000). Eerdmans Dictionary of the Bible. Amsterdam University Press. p. 709. Retrieved 15 February 2014. 
  2. Keith Akers, The lost religion of Jesus: simple living and nonviolence in early Christianity, Lantern Books, 2000 p. 21
  3. Wylen, Stephen M., The Jews in the Time of Jesus: An Introduction, Paulist Press (1995), ISBN 0-8091-3610-4, Pp 190-192.; Dunn, James D.G., Jews and Christians: The Parting of the Ways, A.D. 70 to 135, Wm. B. Eerdmans Publishing (1999), ISBN 0-8028-4498-7, Pp 33–34.; Boatwright, Mary Taliaferro & Gargola, Daniel J & Talbert, Richard John Alexander, The Romans: From Village to Empire, Oxford University Press (2004), ISBN 0-19-511875-8, p. 426.;
  4. Theological dictionary of the New Testament 1972 p568 Gerhard Kittel, Geoffrey William Bromiley, Gerhard Friedrich "When the Jewish Christians whom James sent from Jerusalem arrived at Antioch, Cephas withdrew from table-fellowship with the Gentile Christians:"
  5. Cynthia White The emergence of Christianity 2007 p36 "In these early days of the church in Jerusalem there was a growing antagonism between the Greek-speaking Hellenized Jewish Christians and the Aramaic-speaking Jewish Christians"
  6. Michele Murray Playing a Jewish game: Gentile Christian Judaizing in the first and Second Centuries CE, Canadian Corporation for Studies in Religion - 2004 p97 "Justin is obviously frustrated by continued law observance by Gentile Christians; to impede the spread of the phenomenon, he declares that he does not approve of Jewish Christians who attempt to influence Gentile Christians "to be.. "
  7. McGrath, Alister E., Christianity: An Introduction. Blackwell Publishing (2006). ISBN 1-4051-0899-1. Page 174: "In effect, they [Jewish Christians] seemed to regard Christianity as an affirmation of every aspect of contemporary Judaism, with the addition of one extra belief — that Jesus was the Messiah. Unless males were circumcised, they could not be saved (Acts 15:1)."
  8. 8.0 8.1 8.2 Damick, Fr. Andrew Stephen (2011), Orthodoxy and Heterodoxy, Chesterton, IN: Ancient Faith Publishing, p. 20, ISBN 978-1-936270-13-2 

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wakristo wa Kiyahudi kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.