Vladimir Putin

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Vladimir Putin mwaka 2021.

Vladimir Vladimirovich Putin, (kwa Kirusi Владимир Владимирович Путин; alizaliwa 7 Oktoba 1952) ni mwanasiasa wa nchini Urusi. Mara nne alichaguliwa kuwa Rais wa Shirikisho la Urusi, mara ya mwisho kwenye mwaka 2018; awamu za kwanza zilikuwa kutoka 2000 hadi 2008. Kuanzia Agosti 1999 hadi Mei 2000, tena kuanzia 2008 hadi 2012 alikuwa waziri mkuu wa Urusi. Baadaye aligombea tena uraisi aliporudishwa mwaka 2018.

Alikaimu kiti cha Urais tarehe 31 Desemba 1999, pale rais Boris Yeltsin alipojiuzulu kwa ghafla. Kisha Putin akashinda uchaguzi wa rais mnamo mwaka wa 2000. Mnamo mwaka wa 2004, alichaguliwa upya na kushinda, hivyo aliendelea na kipindi chake cha pili hadi tarehe 7 Mei 2008.

Putin ni Mrusi wa Kanisa la Kiorthodoksi; mama yake alikuwa Mkristo wa kujitolea aliyekuwa akihudhuria katika kanisa wakati baba yake hakuamini Mungu. Mama yake hakuweka usaidizi wowote nyumbani lakini alihudhuria kanisani mara kwa mara japokuwa serikali ilinyanyasa dini yake kwa wakati huo. Mama yake alimbatiza kwa siri akiwa mdogo na mara kwa mara alimpeleka kuabudu.

Katika michezo Putin ameonekana mara kwa mara akiendeleza tasnia ya michezo kama vile kuendesha baiskeli, kutereza kwa ski, badminton.

Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Vladimir Putin kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.