Uwanja wa Taifa (Zimbabwe)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uwanja wa Michezo wa Kitaifa Zimbabwe ni uwanja wa michezo uliopo katika mji wa Harare, nchini Zimbabwe wenye uwezo wa kuchukua watu 60,000.[1] Ni uwanja wa kwanza kwa ukubwa nchini Zimbabwe na unatumika sana kwa ajili ya mchezo wa mpira wa miguu pamoja mchezo wa rugby, pia unatumika kama uwanja wa nyumbani wa timu ya CAPS United F.C..


Mnamo tarehe 20 Novemba 2006 uwanja huu ulifungwa kwa ajili ya marekebisho na ukarabati mkubwa uliochukua takribani miezi 20 kukamilika.[2]

Tarehe 14 Septemba 2019 uwanja ulitumika kwa ajili ya mazishi ya kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Zimbabawe hayati Robert Mugabe,[3][4] mazishi yaliyohudhuriwa na viongozi wengi akiwemo raisi Emmerson Mnangagwa, Dr. Kenneth Kaunda wa Zambia, Olusegun Obasanjo wa Nigeria, Hifikepunye Pohamba na Hage Geingob wa Namibia, Joseph Kabila wa DR Congo, Uhuru Kenyatta wa Kenya na Cyril Ramaphosa wa South Africa.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Machamire, Farayi (4 March 2017). "Zim stadia 'shameful'". DailyNews Live. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-12-07. Iliwekwa mnamo 14 January 2019.  More than one of |accessdate= na |access-date= specified (help); Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  2. BBC SPORT | Football | African | Zimbabwe to renovate main stadium
  3. Burke, Jason. "Pomp, thin crowds and mixed feelings as Robert Mugabe is buried", The Guardian, 15 September 2019. 
  4. Bentley, Cara. "'The end does not justify the means' say Zimbabwean bishops as Mugabe's funeral takes place", Premier Christian Radio, 14 September 2019. 
Makala hii kuhusu mambo ya michezo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu zaidi kuhusu Uwanja wa Taifa (Zimbabwe) kama historia yake, uenezi au kanuni zake?
Labda unaona katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine habari zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.