Stephen Hawking

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
:Stephen_Hawking.StarChild.jpg
Stephen William Hawking

Stephen William Hawking, CH CBE FRS (Oxford, 8 Januari 1942 - Cambridge, 14 Machi 2018) alikuwa mtaalamu wa fizikia na hisabati kutoka Uingereza, mmoja kati ya wataalamu wa fizikia wa kinadharia ulimwenguni.

Aliandika vitabu mashuhuri kuhusu sayansi vinavyolenga watu ambao si wanasayansi.

Hawking alikuwa profesa wa hisabati katika Chuo Kikuu cha Cambridge (nafasi ambayo Isaac Newton aliwahi kuwa nayo). Alistaafu tarehe 1 Oktoba 2009.

Maisha ya awali na elimu[hariri | hariri chanzo]

Mwaka 1950 Hawking alienda Shule ya St Albans, shule ya umma ya Hertfordshire. Akiwa na umri wa miaka 17, alipitia mtihani wa kujifunza huko Oxford. Alijifunza fizikia na kemia huko. Kwa sababu aliona ni rahisi sana mwanzoni, hakujifunza mengi kwa ajili ya mitihani ya mwisho.

Mnamo Oktoba 1962 alianza kozi yake ya kuhitimu katika Trinity Hall. Ulikuwa wakati ugonjwa wake ulianza kujionyesha. Alikuwa na shida katika kujinyoosha na kisha hata tu kutembea. Hata hivyo, alimaliza PhD yake akaandika kuhusu mashimo meusi katika shahada yake. Alipata ushirika (kazi kama mwalimu wa chuo kikuu) katika Chuo cha Gonville na Caius mwaka wa 1965.

Ana ugonjwa wa chembe za neva unaohusiana na ulemavu wa akili unaosababisha mtu kuwa na shida ya kusoma na kuandika (Dyslexia kwa Kiingereza), na kwa sababu hiyo hawezi kutembea au kuzungumza vizuri. Ugonjwa huo ulizidi hata kuwa karibu kabisa na kupooza. Alitumia gurudumu kusonga, na kompyuta ya Intel ili kuzungumza.

Vitabu vyake[hariri | hariri chanzo]

Vitabu vinavyolenga wasomaji wote[hariri | hariri chanzo]

Vitabu kadhaa vya kitaalamu[hariri | hariri chanzo]

Utangulizi wa kitabu[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. "How Physics got Weird", Wall Street Journal, 5 December 2016. 
Makala hii kuhusu mwanasayansi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Stephen Hawking kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.