Sikipi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sikipi
Sikipi wa Afrika
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Galliformes (Ndege kama kuku)
Familia: Phasianidae (Ndege walio na mnasaba na kwale)
Horsfield, 1821
Nusufamilia: Perdicinae
Horsfield, 1821
Ngazi za chini

Jenasi 13 za sikipi:

Sikipi ni ndege wa jenasi mbalimbali katika nusufamilia Perdicinae wa familia Phasianidae. Spishi za Ptilopachus huainishwa katika familia Odontophoridae siku hizi, kwa sababu zina nasaba na tombo wa Dunia Mpya. Ndege hawa wanafanana na kwale na tombo, lakini ukubwa wao ni katikati ya zile za ndege hawa. Hata mwenendo wao ni kama ule wa ndege hawa. Hula mbegu hasa lakini wadudu pia. Hutaga mayai tano hadi zaidi ya kumi ardhini pengine juu ya manyasi makavu.

Sikipi wanatokea Afrika, Ulaya na Asia, lakini sikipi chukar amewasilishwa katika Amerika ya Kaskazini, New Zealand na Hawaii. Spishi nyingi huwindwa sana mahali pengi.

Spishi za Afrika[hariri | hariri chanzo]

Spishi za mabara mengine[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]