Sidney Poitier

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sir Sidney Poitier

Poitier in 1968

Balozi wa Bahamas nchini Japan

tarehe ya kuzaliwa (1927-02-20)Februari 20, 1927
Miami, Florida
tarehe ya kufa 6 Januari 2022 (umri 94)
Bahamas
uraia Bahamas, Marekani
taaluma
  • Mwigizaji
  • Mwongozaji
  • Mwandishi
  • Balozi

Sidney Poitier [1] (20 Februari 19276 Januari 2022) alikuwa mwigizaji, mwongozaji wa filamu, mwandishi na mwanadiplomasia kutoka nchi ya Bahamas.

Mwaka 1964 alikuwa mwigizaji Mweusi wa kwanza kushinda tuzo ya akademi ("Oscar") kwa mwigizaji bora.

Aliigiza katika filamu za Marekani ambazo zilipambana na ubaguzi wa rangi. Kazi yake ilichangia sana kufanya waigizaji Weusi kuheshimiwa zaidi katika biashara ya sinema.

Kuanzia 1997 hadi 2007, alikuwa balozi wa Bahamas nchini Japani .

Maisha ya awali[hariri | hariri chanzo]

Wazazi wa Poitier walikuwa Evelyn na Reginald James Poitier[2]. Walikuwa wakulima kwenye kisiwa cha Cat cha Bahamas[3]. Walienda mara kwa mara Miami, Florida kuuza mazao huko na katika safari mojawapo Sidney alizaliwa huko Miami. Kwa sababu hiyo alipata pia uraia wa Marekani[4].

Alipokuwa na umri wa miaka 15, wazazi wa Poitier walimtuma Miami kuishi na kaka yake mkubwa. Akiwa na umri wa miaka 17, alihamia New York City na kutafuta kazi ndogondogo. Aliamua kujiunga na Jeshi la Marikani alipokaa kwa muda mfupi tu. Alipewa kazi ya kuwahudumia wagonjwa katika hospitali ya kijeshi lakini hakupenda jinsi hospitali ilivyowatendea wagonjwa. Aliachishwa kwa sababu za kiafya. Baadaye alifanya kazi ya kuosha vyombo hadi akapata kazi katika jumba la tamthilia la American Negro Theater.

Kazi ya uigizaji[hariri | hariri chanzo]

Poitier, Harry Belafonte, na Charlton Heston kwenye Maandamano kwa Washington, 1963

Poitier alishindwa kutofautisha sauti za muziki hivyo hakuweza kuimba au kucheza kwenye jukwaa. Hivi ndivyo waigizaji weusi walifanya wakati huo, kwa hivyo watazamaji hawakumpenda. [5] Alifanya kazi kwa bidii sana ili kuboresha ujuzi wake wa uigizaji, na kuondokana na lafudhi yake ya Kibahama. Hatimaye alipata nafasi ya kuigiza katika tamthilia Lysistrata kwenye jukwaa moja ya Broadway na wahakiki wa magazeti walimpenda. Mwishoni mwa mwaka 1949, alipata nafasi katika filamu No Way Out (1950) iliyongozwa na Darryl F. Zanuck. Alimwigiza daktari anayemtibu mtu mweupe aliye mnafiki wa dini. Baada ya kazi hii, alifaulu kupata majukumu zaidi ya filamu. Nafasi za uigizaji alizopata zilikuwa bora na za kuvutia zaidi kuliko majukumu ya waigizaji wengi weusi wakati huo.

Poitier alikuwa mwigizaji wa kwanza mweusi kushinda Tuzo la Akademi la Mwigizaji Bora (kwa Lilies of the Field mnamo 1963). [6]

Baadaye Poitier alianza kukosolewa kwa kuigiza nafasi za wahusika weusi wenye tabia nzuri pekee. Poitier alikubaliana na hili lakini ijapokuwa alitaka majukumu tofauti zaidi, lakini pia alitaka kuonyesha mfano mzuri na wahusika wake na kwenda kinyume na dhana mbaya zilizokuja hapo awali kihusu wahusika weusi katika tasnia ya sinema. Alikuwa mwigizaji mkuu pekee mweusi katika tasnia ya sinema ya Marekani wakati ule.

Kazi ya mwongozaji[hariri | hariri chanzo]

Poitier ameongoza filamu kadhaa. Iliyofanikiwa zaidi ilikuwa kichekesho cha Stir Crazy . Filamu ya kwanza aliyoiongoza ilikuwa filamu ya western Buck and the Preacher . Humo alikuwa pia na nafasi pamoja na Harry Belafonte . Filamu nyingine alizoziongoza ni Uptown Saturday Night, Let's Do It Again, A Piece of the Action, na Ghost Dad .

Maisha binafsi[hariri | hariri chanzo]

Poitier, Mary Robinson, na Desmond Tutu wanakaribia kupokea Nishani ya Rais ya Uhuru, 2009

Poitier alioa mara mbili; mke wa kwanza alikuwa Juanita Hardy kutoka 29 Aprili 1950 hadi 1965. Mke wake wa pili ni Joanna Shimkus, mwigizaji kutoka nchini Kanada, tangu Januari 1976. Alipata mabinti wanne kwa ndoa yake ya kwanza na wawili wa pili.

Maisha ya baadaye[hariri | hariri chanzo]

Mnamo Aprili 1997, Poitier alikuwa balozi wa Bahamas nchini Japani. Pia alikuwa balozi wa Bahamas katika UNESCO. Kuanzia 1998 hadi 2003, alikuwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Walt Disney. [7]

Mnamo 2001, Poitier alipokea Tuzo la Heshima la Akademi kwa mchango wake wa jumla katika sinema ya Amerika. Mnamo Agosti 2009, alipokea Nishani ya Uhuru kutoka kwa Rais Barack Obama .

Poitier alikufa mnamo Januari 6, 2022 huko Bahamas, akiwa na umri wa miaka 94. [8]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Because Poitier is a citizen of The Bahamas, a Commonwealth realm, this is a substantive (as opposed to honorary) knighthood, which entitles him to the style "Sir". However, Poitier employs the title only in connection with his official ambassadorial duties.
  2. Sidney Poitier Biography (1927-)
  3. "Tavis Smiley interviews Sidney Poitier". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2009-03-16. Iliwekwa mnamo 2017-08-31. 
  4. Adam Goudsouzian, Sidney Poitier: Man, Actor, Icon (2004), p.8.
  5. Goudsouzian; Sidney Poitier; pp. 69, 133
  6. On This Day: 1964: Poitier breaks new ground with Oscar win at BBC News.com
  7. Actor Takes Center Stage as Disney Trial Grinds On
  8. Sidney Poitier: Hollywood star dies aged 94

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]