Sanje

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Sanje ni kata inayopatikana katika tarafa ya Kidatu, wilaya ya Ifakara Mjini, Mkoa wa Morogoro, Tanzania yenye Postikodi namba 67507.

Kata ya Sanje ipo kando ya safu za Milima ya Udzungwa na ina vivutio vya utalii ambavyo baadhi yake vinavyopatikana katika milima hiyo kama vile maporomoko ya maji ya Sanje (Sanje Waterfalls) na wanyama jamii ya nyani wanaofahamika kama mbega.

Kata hiyo inajumlisha vijiji vitatu ambavyo ni Sanje, Msolwa Ujamaa na Miwangani. Jina la kata limetokana na uwepo wa kijiji cha Sanje chenye vitongoji kama Shuleni, Barabarani, Mpirani na Udzungwa.

Kadiri ya sensa ya mwaka 2022 kata ina jumla ya wakazi 12,777 [1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 11,041 [2] walioishi humo.

Wakazi wa kata hiyo hujishughulisha zaidi na kilimo cha mazao ya biashara kama miwa kwa wingi ambayo waiuza katika kiwanda cha miwa cha Kilombero Sugar Company Limited, na mpunga. Pia hulima mazao mengine kama mahindi na viazi vitamu.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.nbs.go.tz
  2. "Sensa ya 2012, Morogoro - Kilombero DC". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2016-03-03. Iliwekwa mnamo 2016-06-03. 
Kata za Wilaya ya Ifakara Mjini - Mkoa wa Morogoro - Tanzania

Ifakara | Katindiuka | Kibaoni | Kiberege | Kidatu | Kisawasawa | Lipangalala | Lumemo | Mang'ula | Mang’ula 'B' | Mbasa | Michenga | Mkula | Mlabani | Msolwa Station | Mwaya | Sanje | Signal | Viwanjasitini


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Morogoro bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Sanje kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa na viongozi wa sasa maana wanabadilika haraka mno.