Salome (mke wa Zebedayo)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Salome)
Picha takatifu ya Kiorthodoksi ya Salome na wenzake kwenye Kaburi la Yesu (Kizhi, karne ya 18).

Salome (kwa Kiebrania: שלומית, Shelomit, kutoka mzizi שָׁלוֹם, shalom, yaani amani[1]) alikuwa mke wa Zebedayo na mfuasi wa Yesu Kristo pamoja na wanae Yakobo Mkubwa na Mtume Yohane, waliokuwa marafiki wakuu wa Yesu pamoja na mtume Petro.

Kwa msingi huo alithubutu kumuomba Yesu awape wanae nafasi mbili za kwanza katika ufalme wake ujao.

Anatajwa kati ya wanawake waliosimama chini ya Yesu msalabani (Mk 15:40; Math 27:56) na kati ya wale waliowahi kwenda kaburini Jumapili asubuhi na mapema (Mk 16:1)[2].

Pengine anadhaniwa kuwa na undugu na Bikira Maria, mama wa Yesu.[3]

Anaheshimiwa na madhehebu mengi ya Ukristo kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 24 Aprili.[4]

Picha[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Salome (mke wa Zebedayo) kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.