Rikitrude

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya Mt. Rikitrude huko Boiry-Sainte-Rictrude.

Rikitrude (pia: Rictrude, Rictrudis, Richtrudis, Richrudis; 612 - 12 Mei 688) alikuwa mwanamke wa ukoo maarufu wa Ufaransa Kusini Magharibi ambaye tangu ujanani aliongozwa kiroho na Amando akaolewa na Adalbati I akaishi naye maisha maadilifu sana[1][2] .

Baada ya mumewe kuuawa, kwa ushauri wa Amando alijiunga na monasteri ya Marchiennes aliyokuwa ameianzisha, akawa abesi wake[3] na kuongoza vizuri sana mabikira waliowekwa wakfu huko[4].

Anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu, sawa na mume wake na watoto wao wote wanne, Klotsinda, Adalsinda, Eusebia wa Douai na Morandi.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 12 Mei[5].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Karine Ugé, The Legend of Saint Rictrude, pp. 283-4, in John Gillingham, Anglo-Norman Studies 23: Proceedings of the Battle Conference 2000 (2001)
  2. Philip Lyndon Reynolds, Marriage in the Western Church (2001), p. 411.
  3. Cristiani, Léon. "Liste chronologique des saints de France, des origines à l'avènement des carolingiens", Revue d'histoire de l'Église de France, 1945, p. 76
  4. http://www.santiebeati.it/dettaglio/92778
  5. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Jo Ann McNamara, John E. Halborg, E. Gordon Whatley (1992), Sainted Women of the Dark Ages, pp. 195–219

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.