Petro wa Betancur

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sanamu ya Petro wa Mt. Yosefu Betancur katika Pango la Mt. Hermano Pedro (Tenerife).

Petro wa Betancur (Tenerife, Hispania, 21 Machi 1626 - Antigua, Guatemala 25 Aprili 1667), alikuwa mmisionari kutoka Hispania katika Amerika ya Kati.

Alijulikana kama "Mt. Fransisko wa Amerika", naye ni mtakatifu wa kwanza mzaliwa wa funguvisiwa la Kanaria, pia anahesabiwa wa kwanza katika Guatemala na Amerika ya Kati kwa jumla.

Petro alitambulikana kwa unyenyekevu na ugumu wa maisha katika kutekeleza huruma kwa wengine, wakiwemo mayatima, watoto wa mitaani, vijana wasioelimika, ombaomba, wagonjwa,, wageni na waliohukumiwa kufanya kazi za shokoa.[1]

Mwanashirika wa Utawa wa Tatu wa Mt. Fransisko, alianzisha pia shirika la kwanza la barani Amerika, "Ndugu wa Kiume na wa Kike wa Bethlehemu". Baada ya kufutwa, lilifufuliwa tarehe 16 Januari 1984.

Alitangazwa na Papa Yohane Paulo II kuwa mwenye heri tarehe 22 Juni 1980, halafu mtakatifu tarehe 30 Julai 2002. [1]

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 25 Aprili[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.