Watoto wa mitaani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Watoto wakilala katika Mulberry Street, New York City, 1890.
Watoto wa mitaani huko Kabul, Afghanistan.

Watoto wa mitaani ni watoto ambao wamekosa makazi bora, malazi na mavazi kutoka kwa wazazi au walezi wao. Jambo hilo limesababisha kutokuwa na mahali maalumu pa kuishi.

Idadi yao duniani hukadiriwa kuwa milioni mia moja hivi.

Sababu[hariri | hariri chanzo]

Kuwa mtoto wa mitaani husababishwa na ugomvi wa wazazi ambao hatimaye hutengana; hapo mtoto hukosa haki na mahitaji yake ya msingi. Mtoto huona bora akaishi mtaani ili aweze kufanya japo kazi ndogo aweze kupata mahitaji yake.

Pengine hutokana na vifo vya wazazi wote wawili, ambapo baadhi yao hutengwa na ndugu na kukosa mahali pa kwenda.

Kuna wakati watoto hao hukosa chakula, hivyo huona bora aibe ili apate kula. Wengine huingia kwenye makundi ya uuzaji wa madawa ya kulevya na ujambazi.

Majukumu[hariri | hariri chanzo]

Jamii inatakiwa ichukue jukumu la kuwasaidia watoto haO ili kuwaepusha na mambo hayo. Sisi sote kama jamii tunatakiwa tuliangalie suala hilo kwa umakini kwa usaidizi wa serikali; jukumu hili ni la kila mtu.

Ingawa serikali nyingine zimetekeleza mipango ya kukabiliana na matatizo ya watoto wa mitaani, mpaka sasa suluhisho la jumla linahusisha kuwaweka katika makazi ya mayatima, nyumba za vijana, au taasisi za marekebisho.

Huko Kolombia, serikali imejaribu kutekeleza mipango ya kuweka watoto hawa katika nyumba zinazoendeshwa na serikali, lakini jitihada hizo zimeshindwa kwa kiasi kikubwa, na watoto wa mitaani wamekuwa kundi la watu walioathiriwa na ukatili wa Polisi na Usalama wa Taifa, kwa sababu, wanadhani ni watumiaji wa madawa ya kulevya na wahalifu.

Katika Australia, majibu ya msingi kwa wasio na makazi ni Programu ya Usaidizi wa Makazi ya Usaidizi (SAAP). Mpango huo ni mdogo kwa ufanisi wake. Inakadiriwa moja kati ya vijana wawili ambao wanatafuta kitanda kutoka SAAP hugeuzwa kwa sababu huduma zimejaa.

Jitihada za kufaa zaidi zimefanywa na serikali mbalimbali kusaidia au kushirikiana na mashirika yasiyo ya serikali.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: