Paulo Hanh

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Paulo Hanh (kwa Kivietnam: Phaolô Hạnh; Chợ Quán, Vietnam, 1826 hivi - Saigon, Vietnam, 28 Mei 1859) alikuwa Mkristo ambaye, baada ya kupuuzia maadili, aliongoza kikundi cha majambazi.

Alipokamatwa chini ya kaisari Tu Duc, alikiri kwa ushujaa imani yake bila kujali mabembelezo, vitisho na mateso hata akakatwa kichwa[1] na hivi kuwa mmojawapo kati ya Wakristo wafiadini wa Vietnam waliouawa kwa ajili ya imani yao huko Vietnam katika karne ya 17, 18 na 19 (16251886).

Wanatajwa pia kama Watakatifu Andrea Dũng-Lạc na wenzake 116.

Kwa nyakati tofauti, Papa Leo XIII, Papa Pius X na Papa Pius XII waliwatangaza kuwa wenye heri, halafu Papa Yohane Paulo II aliwaunganisha katika kuwafanya watakatifu wafiadini tarehe 19 Juni 1988.

Sikukuu yao huadhimishwa kwa pamoja kila tarehe 24 Novemba. Paulo Hahn anaadhimishwa pia tarehe 28 Mei, ambapo ndipo alipouawa akiwa mlei[2].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/55010
  2. Martyrologium Romanum

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Les Missions Etrangères. Trois siecles et demi d'histoire et d'aventure en Asie Editions Perrin, 2008, ISBN 978-2-262-02571-7
  • "St. Andrew Dung-Lac & Martyrs", by Father Robert F. McNamara, Saints Alive and All God's Children Copyright 1980-2010 Rev. Robert F. McNamara and St. Thomas the Apostle Church.
  • "Vietnamese Martyr Teaches Quiet Lessons", By Judy Ball, An AmericanCatholic.org Web Site from the Franciscans and St. Anthony Messenger Press.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.