Paulo Burali

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Paulo (Scipione) Burali wa Arezzo.

Paulo Burali wa Arezzo (Itri, Lazio, Italia, 1511Torre del Greco, Campania, Italia, 17 Juni 1578) alikuwa askofu mkuu wa Napoli na kardinali kutoka shirika la Wateatini.

Ujuzi wake wa sheria ulimpa vyeo vikubwa katika mahakama za Napoli pamoja na nafasi za kutetea haki za wananchi.

Hata hivyo aliacha kila kitu ili kufuata wito wake wa kitawa. Alipewa upadrisho tarehe 26 Machi 1558.

Baada ya kushika uongozi shirikani, Papa Pius V alimfanya kardinali tarehe 17 Mei 1570, halafu chini ya Papa Gregori XIII alipewa askofu tarehe 4 Julai 1572 akaongoza jimbo kuu la Napoli miaka 1576-1578.

Pamoja na ukali wake, alichangia sana urekebisho wa Kikatoliki nchini Italia.

Papa Klementi XIV alimtangaza mwenye heri tarehe 18 Juni 1772.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]


Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Paolo Burali (Catholic-Hierarchy)
  • Biography (Salvador Miranda)
  • Epistolario del beato Paolo Burali: cardinale teatino, vescovo di Piacenza, arcivescovo di Napoli (1511-1578) (Brescia: Centro bresciano di iniziative culturali, 1977).
  • Piacenza e il B. Paolo Burali: atti del convegno di studio in occasione del IV centenario dalla morte (Deputazione di storia patria per le province parmensi, 1979) [Archivio storico per le province parmensi 4th series, Vol. 30, t. 2].
  • Franco Molinari, Il Card. Teatino Beato Paolo Burali e la riforma tridentina a Piacenza (1568-1578) (Rome: Gregorian University 1957) [Analecta Gregoriana 87].
  • Andrea Avellino, Brevi cenni sulla vita del Beato Paolo Burali d'Arezzo seconda edizione (Napoli 1876).
  • G. B. Maffi, Vita del Beato Paolo d' Arezzo (Piacenza 1833).
  • G. B. Bonaglia, Vlta del Beato Paolo Burali d' Arezzo, Chierico Regolare, Cardinale di S. Pudenziana (Napoli 1772).
  • Giovanni Bonifacio Bagata, CR, Vita del Venerabile Paolo Burali d'Arezzo (Verona 1698).
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.