Pasiano

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Pasiano kadiri ya Joan Roig na Joan Moxí.

Pasiano (Hispania, 310 hivi - Barcelona, Hispania, 391 hivi) alikuwa askofu wa 2 wa mji huo kuanzia mwaka 365 hadi kifo chake.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu na babu wa Kanisa[1].

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 9 Machi[2].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Aliwahi kuoa na kuzaa mtoto aliyefanya kazi ikulu.

Jeromu alisifu maisha yake matakatifu pamoja na usafi wa moyo, ujuzi na ufasaha[3].

Katika kuhubiri alikuwa akisema jina lake ni Mkristo na ubini wake ni Mkatoliki[4].

Maandishi[hariri | hariri chanzo]

Aliandika kuhusu mada mbalimbali, lakini vimetufikia kitabu kimoja juu ya toba na barua tatu tu[5].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.