Pansofi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Pansofi (alifariki 250 hivi) alikuwa Mkristo wa Misri ambaye aliteswa na hatimaye kufia dini yake wakati wa dhuluma ya kaisari Decius[1].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Mtoto wa gavana wa Aleksandria, Misri, aliporithi mali ya baba yake, aliigawa yote kwa mafukara akaenda kuishi kama mkaapweke kwa miaka 20.

Sifa yake ya utakatifu ilimfanya akamatwe na kuuawa dhuluma mpya ilipoanza.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 15 Januari.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.