Pambo wa jangwani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Pambo wa Nitria.

Pambo wa jangwani (kwa Kigiriki: Όσιος Παμβώ; kwa Kiarabu-Kikopti: موا au بيموا, Pemwah au Bemwah; alifariki 375 hivi) ni kati ya Wakristo wa Misri waliokwenda kuishi jangwani chini ya Antoni Mkuu[1]. Baadaye alianzisha monasteri nyingi.[2]

Alijulikana kwa hekima yake akaombwa shauri na wengi, wakiwemo Athanasius, Melania Mzee na Rufinus.

Kati ya wanafunzi wake wamo Pishoy na Yohane Mbilikimo.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 1 Julai au 18 Julai[3][4][5].

Misemo yake[hariri | hariri chanzo]

Misemo yake katika tafsiri ya Kiswahili inapatikana ndani ya kitabu:

  • Misemo ya Mababa wa Jangwani (Apophthegmata Patrum) – tafsiri ya W. Ngowi, O.F.M.Cap. – ed. Salvatorianum – Morogoro 2000ISBN 0-264-66350-0

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. As a youngster, Saint Pambo once asked Saint Anthony "My Father, teach me to live well." To which the great Saint Anthony answered "My son, to live well, one must have a great distrust of oneself, with every effort watch over one's heart and mind, and in all things seek God alone." Translation from Jugendspiegel Ludwig Donin, Amberg 1876, Saint Pambo 6 September
  2.  "Thebaid". Catholic Encyclopedia. New York: Robert Appleton Company. 1913.
  3. Saint Pambo, Patron Saints Index, SQPN.
  4. "Преподобный Памва Нитрийский", "Pravoslavie.RU", in Russian.
  5. https://catholicsaints.info/saint-pambo-of-the-nitrian-desert/
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.