Mkoa wa Timbuktu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya Mkoa wa Timbuktu (kabla ya kutengwa kwa Mkoa wa Taoudenit)

Mkoa wa Timbuktu (Kifaransa: Region de Tombouctou; Kibambara : Tumutu Dineja) ni mojawapo ya mikoa ya kiutawala ya Mali. Kabla ya kutengwa kwa Mkoa wa Taoudenit ilikuwa mkoa mkubwa zaidi kati ya mikoa ya Mali ikijumuisha sehemu kubwa ya eneo lake ni Jangwa la Sahara . Kwa madhumuni ya kiutawala, eneo limegawanywa katika wilaya (cercles) tano.

Eneo hilo ni sehemu ya kaskazini mwa Mali ambayo ilitenganishwa na kutangazwa kuwa huru na Harakati ya Kitaifa kwa Ukombozi wa Azawad (MNLA) wakati wa uasi wa Watuareg wa 2012 . Baada ya kutangaza uhuru, MNLA ilishindwa katika mapigano na wanamgambo wa Kiislamu.

Mkoa wa Timbuktu ni maarufu kwa mji mkuu wake ambao ni mji wa kale wa Timbuktu (Kifaransa: Tombouctou).

Mji huo ulipata umaarufu duniani mwaka wa 1390 wakati mtawala wake, Mansa Musa, alipoenda kuhiji Makka, akisimama na msafara wake huko Misri na kutoa dhahabu ya kutosha ili kupunguza thamani ya pesa ya Misri. Hii ilianza hekaya ya jiji lililopo ndani ya bara la Afrika, ambapo barabara zilisemekana kujengwa kwa dhahabu na majengo yaliyoezekwa kwa paa za dhahabu. 

Historia[hariri | hariri chanzo]

Mji uko kwenye ukingo wa kusini wa Sahara, karibu na Mto Niger. Utajiri wa ufalme huo ulitokana na nafasi ya Timbuktu kama kituo cha kusini cha njia ya biashara ya ng'ambo ya Sahara iliyokuwa ya dhahabu, chumvi, njugu za kola, shaba na watumwa.

Utajiri wa Timbuktu ulianza kuporomoka baada ya kutekwa na jeshi la Moroko mnamo 1592. Wanazuoni wengi wa Kiislamu walitawanywa, wengine hadi Moroko.

Hatimaye ilikuwa ni kuongezeka kwa biashara ya baharini kwenye pwani ya Afrika Magharibi ambayo ilipunguza umuhimu wa njia za nchi kavu zilizounganisha Afrika Kaskazini na Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara. Mji ulipoteza msingi wake wa kiuchumi na chuo kikuu chake kizuri hakikutosha kuokoa Timbuktu kutokana na kushuka.

Eneo hili lilishuka zaidi kiuchumi wakati wa ukoloni ya Kifaransa uliomalizika mnamo 1960. Wafaransa walifungua njia fupi za biashara hadi Atlantiki, na hivyo kumaliza yale yaliyowahi kubaki na uchumi wa biashara ya kuvuka Sahara.

Wilaya (cercles) za Mkoa wa Tombouctou (kabla ya kutengwa kwa Mkoa wa Taoudenit)

Wilaya[hariri | hariri chanzo]

Mkoa umegawanywa katika wilaya (cercles) tano : [1] [2]

Jina la Cercle Eneo (km2) Idadi ya watu
(Sensa ya 1998)
Idadi ya watu
(Sensa ya 2009)
Niafunke 12,000 119,900 184,285
Dire 1,750 76,960 111,324
Goundam 92,688 113,897 150,150
Tombouctou 347,488 68,228 124,546
Gourma-Rharous 45,000 63,634 111,386

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Loi N°99-035/ du 10 Aout 1999 Portant Création des Collectivités Territoriales de Cercles et de Régions (in French), Ministère de l'Administration Territoriales et des Collectivités Locales, République du Mali, 1999, archived from the original on 2012-03-09 .
  2. Communes de la Région de Tombouctou (in French), Ministère de l’administration territoriale et des collectivités locales, République du Mali, archived from the original on 2012-09-19 .