Lugha za Kihindi-Kiajemi

Lugha za Kihindi-Kiajemi ni kundi kubwa zaidi katika familia ya lugha za Kihindi-Kiulaya. Zinajumuisha lugha za Kihindi-Kiarya na lugha za Kiajemi (Irani). Zinazungumzwa zaidi kwenye Bara Hindi na Nyanda za Juu za Iran. Hapo zamani zilitumiwa pia katika Asia ya Kati, mashariki mwa Bahari ya Kaspi .
Lugha za Kihindi-Kiarya[hariri | hariri chanzo]
Kuna karibu lugha 221 za Kihindi-Kiarya (Indic), zenye jumla ya wasemaji zaidi ya milioni 800.
- Kibengali (lugha rasmi nchini Bangladesh; lugha rasmi ya jimbo la Bengala Magharibi nchini Uhindi)
- Kimarathi (lugha rasmi ya jimbo la nchini Uhindi)
- Kihindustani (kwa umbo la Kiurdu: lugha rasmi nchini Pakistan; lugha rasmi ya kieneo nchini Uhindi pamoja na Kihindi, aina nyingine ya Kihindustani)
Lugha za Kiajemi (Kiirani)[hariri | hariri chanzo]
Kuna karibu lugha 86 za Kiajemi, zenye wasemaji kati ya milioni 150 hadi 200.
- Kiajemi (lugha rasmi nchini Iran; pia rasmi kwa jina la Dari nchini Afghanistan na kama Kitajiki huko Tajikistan)
- Kipashto (lugha rasmi nchini Afghanistan)
- Kikurdi (lugha rasmi katika eneo la Kurdistan nchini Iraq)
Kinuristani, Kibangani, na Kibadeshi[hariri | hariri chanzo]
Wasomi wengine huchukulia lugha za Kinuristani na Kibangani kama sehemu ya kikundi kidogo cha Kihindi-Kiarya, lakini wengine wanazichukulia kama vikundi viwili tofauti vya Kihindi-Kiajemi. Lugha ya Kibadeshi pia ni lugha ya Kihindi-Kiajemi isiyopangwa bado kimakundi.
Vyanzo[hariri | hariri chanzo]
- Cardona, George. "Indo-Iranian languages". Indo-Iranian languages. https://www.britannica.com/topic/Indo-Iranian-languages. Retrieved 27 August 2018.
- Indo-Iranian.