Lugha za Kihindi-Kiajemi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Lugha za Kihindi-Kiulaya; buluu: maeneo ya lugha za Kihindi-Kiajemi

Lugha za Kihindi-Kiajemi ni kundi kubwa zaidi katika familia ya lugha za Kihindi-Kiulaya. Zinajumuisha lugha za Kihindi-Kiarya na lugha za Kiajemi (Irani). Zinazungumzwa zaidi kwenye Bara Hindi na Nyanda za Juu za Iran. Hapo zamani zilitumiwa pia katika Asia ya Kati, mashariki mwa Bahari ya Kaspi .

Lugha za Kihindi-Kiarya[hariri | hariri chanzo]

Kuna karibu lugha 221 za Kihindi-Kiarya (Indic), zenye jumla ya wasemaji zaidi ya milioni 800.

Lugha za Kiajemi (Kiirani)[hariri | hariri chanzo]

Kuna karibu lugha 86 za Kiajemi, zenye wasemaji kati ya milioni 150 hadi 200.

Kinuristani, Kibangani, na Kibadeshi[hariri | hariri chanzo]

Wasomi wengine huchukulia lugha za Kinuristani na Kibangani kama sehemu ya kikundi kidogo cha Kihindi-Kiarya, lakini wengine wanazichukulia kama vikundi viwili tofauti vya Kihindi-Kiajemi. Lugha ya Kibadeshi pia ni lugha ya Kihindi-Kiajemi isiyopangwa bado kimakundi.

Vyanzo[hariri | hariri chanzo]