Koloni la Rasi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Koloni ya Rasi)
Cape Colony - Kaapkolonie
Koloni ya Rasi
Bendera ya Koloni ya Rasi
Bendera ya Koloni ya Rasi
Lugha rasmi Kiingereza na Kiholanzi 1
Mji mkuu Cape Town
Eneo 569,020 km² (1910)
Koloni ya Rasi katika Muungano wa Afrika Kusini
Koloni ya Rasi katika Muungano wa Afrika Kusini
1 Hadi 1806 Kiholanzi ilikuwea lugha rasmi pekee; kati ya 1806 na 1882 Kiingereza. Tangu 1882 lugha zote mbili zilikuwa lugha rasmi.

Koloni la Rasi lilikuwa koloni la Uholanzi kuanzia mwaka 1652 hadi 1806 na baadaye la Uingereza kuanzia 1806 hadi 1910. Jina limetokana na Rasi ya Tumaini Jema iliyoko karibu na mji wa Cape Town katika Afrika Kusini ya leo.

Koloni la Uholanzi[hariri | hariri chanzo]

Historia ya koloni ilianza mwaka 1652 wakati Mholanzi Jan van Riebeeck aliunda Cape Town kwa niaba ya Kampuni ya Kiholanzi kwa India ya Mashariki. Kampuni hiyo ilihitaji kituo kwa ajili ya jahazi zake zilizosafiri kati ya Ulaya na visiwa vya Indonesia. Eneo la rasi lilifaa kuwa mahali pa kupumzika na kuongeza vyakula njiani tena kwa sababu hali ya hewa iliwafaa watu wa Ulaya.

Waholanzi walipeleka wakulima kwenda rasi waliotakiwa kulima vyakula kwa ajili ya mahitaji ya jahazi.

Koloni la Uingereza[hariri | hariri chanzo]

Wakati wa vita za Napoleoni eneo la Uholanzi lilitawaliwa na Ufaransa na Uingereza ilivamia makoloni ya Uholanzi pamoja na rasi. Waingereza waliogopa ya kwamba Wafaransa wangehatarisha mawasiliano na makoloni yao huko Uhindi kama wangetwaa Afrika Kusini. Baada ya miaka kadhaa Waingereza walinyang'anya rasmi eneo hilo mwaka 1806. Hali hii ilitambuliwa na Uholanzi mwaka 1815 kwenye Mkutano wa Vienna.

Koloni la Rasi liliendelea chini ya Uingereza hadi 1910. Mwaka ule Muungano wa Afrika Kusini uliundwa na rasi iliingia ndani yake kama "Jimbo la Rasi".