Harun ar-Rashid

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sarafu ya Dirham yenye jina la Harun ar-Rashid.
Picha ya Harun ar-Rashid katika kitabu cha Alfu Lela U Lela (si sura halisi maana ilichorwa karne kadhaa baadaye).

Harun ar-Rashid (kwa Kiarabu ‏ هارون الرشيد‎) alikuwa khalifa wa tano wa nasaba ya Waabbasi aliyetawala milki kubwa ya Kiislamu (zaidi ya Iran, Iraq, Saudi Arabia, Syria na Afrika Kaskazini) kati ya miaka 786 hadi 809 BK.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Alizaliwa mjini Ray (Uajemi) akafariki mjini Tus (Uajemi) wakati wa vita dhidi ya waasi.

Kipindi chake cha utawala kilikuwa na maendeleo makubwa ya elimu na utamaduni. Sanaa ya Kiislamu (ikiwa pamoja na muziki) ilistawi.

Maktaba yake ilikuwa msingi kwa taasisi ya Nyumba ya hekima (Dar-al-Hikma) mjini Baghdad iliyokuwa kama chuo kikuu ambako vitabu vingi vilitafsiriwa kwa lugha ya Kiarabu kutoka Kigiriki, Kichina, Kisanskrit, Kiajemi na Kiaramu (Syriac). Kwa njia hiyo Baghdad ilikuwa kitovu cha elimu cha kimataifa wakati huo.

Harun alituma mabalozi kwenda hadi China na pia kwa Kaisari Karolo Mkuu wa Dola Takatifu la Kiroma.

Mwaka 796 Harun ar-Rashid alihamisha mji mkuu wake kutoka Baghdad kwenda Raqqa katika Syria.

Anakumbukwa kama mtu wa hekima kubwa, akionekana hivyo katika hadithi za Alfu Lela U Lela.

Vitabu juu ya Harun ar-Rashid[hariri | hariri chanzo]

  • al-Masudi, The Meadows of Gold, The Abbasids, transl. Paul Lunde and Caroline Stone, Kegan paul, London and New York, 1989
  • al-Tabari "The History of al-Tabari" volume XXX "The 'Abbasid Caliphate in Equilibrium" transl. C.E. Bosworth, SUNY, Albany, 1989.
  • Clot, André (1990). Harun Al-Rashid and the Age of a Thousand and One Nights. New Amsterdam Books. ISBN 0-941533-65-4. 
  • Harry St John Bridger Philby. Harun al Rashid (London: P. Davies) 1933.
  • Einhard and Notker the Stammerer, "Two Lives of Charlemagne," transl. Lewis Thorpe, Penguin, Harmondsworth, 1977 (1969)
  • John H. Haaren, Famous Men of the Middle Ages [1]
  • William Muir, K.C.S.I., The Caliphate, its rise, decline, and fall [2]
  • Theophanes, "The Chronicle of Theophanes," transl. Harry Turtledove, University of Pennsylvania Press, Philadelphia, 1982
  • Norwich, John J. (1991). Byzantium: The Apogee. Alfred A. Knopf, Inc. ISBN 0-394-53779-3. 
  • Zabeth, Hyder Reza (1999). Landmarks of Mashhad. Alhoda UK. ISBN 964-444-221-0.