Eutimi abati

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha takatifu ya Mt. Eutimi.

Eutimi abati (pia: Eutimi mkuu; Melitene, Armenia, leo nchini Uturuki, 377[1][2] - 20 Januari 473) alikuwa mmonaki tangu utotoni, halafu padri na hatimaye abati nchini Palestina, alipokwenda kwa siri akiwa na umri wa miaka 30.

Hadi kifo chake alikuwa na unyenyekevu na upendo mkubwa, pamoja na kufuata nidhamu. Kutokana na umaarufu wake, alihamahama sehemu mbalimbali za nchi hiyo ili kukwepa umati uliomtafuta upwekeni[3][4][5][6].

Alipinga uzushi wa Eutike uliolaaniwa na mtaguso wa Kalsedonia (451) akafanya wamonaki wengi na hata malkia wamfuate katika imani sahihi.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 20 Januari [7].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Lives of all saints commemorated on January 9
  2. "Venerable Euthymius the Great", Orthodox church in America
  3. Attwater, Donald and Catherine Rachel John. The Penguin Dictionary of Saints. 3rd edition. New York: Penguin Books, 1993. ISBN|0-14-051312-4.
  4. Ott, Michael. "St. Euthymius." The Catholic Encyclopedia. Vol. 5. New York: Robert Appleton Company, 1909. 21 Jan. 2013
  5. Amnon Ramon, Around the Holy City, p. 67. The Jerusalem Institute for Israel Studies, 2000. Jalada kutoka ya awali juu ya 2017-01-06. Iliwekwa mnamo 2020-04-14.
  6. Euthymius and his monastery in the Judean Desert Yizhar Hirschfeld, Israel Antiquities Authority
  7. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.